Nashukuru UNICEF imenitoa kwenye mgodi hatarishi- Mtoto Clement
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto limechukua hatua kuwaondoa watoto wachimbaji madini kwenye eneo la Kipushi, jimboni Katanga-Juu na kuwapeleka shuleni, hatua ambayo imeleta furaha kwa watoto hao.