Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Msanii akichora picha kwenye ukuta jinsi ya mbinu za mtu kujikinga dhidi ya virusi vya COVID-1 nchini Jamhuri ya afrika ya kati, CAR..
MINUSCA/Screenshot

Nchi za Afrika ya Kati zimedhibiti vyema COVID-19-UN

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika ukanda wa Afrika ya Kati François Louncény Fall amehutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kusema kuwa harakati za serikali kwenye ukanda huo pamoja na wadau wao kukabili janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 zimewezesha ukanda huo kuwa wenye idadi ndogo zaidi ya wagonjwa na vifo vitokanavyo na ugonjwa huo barani Afrika.

 

Janga la Corona limeathiri namna watu wanapitia hedhi salama.
©UNICEF/UNI328066/Nzenze

Wanawake na wasichana wakimbizi wahaha kupata taulo za kike DRC, UNHCR yawasaidia 

Wanawake na wasichana wakimbizi waliotawanywa na machafuko nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC wamekuwa wakiteseka kwa muda mrefu kupata taulo za kike kila mwezi kutokana na gharama huku wakijaribu kulinda uhai wao na kuhudumia familia zao baada ya kukimbia vita. Lakini sasa kwa msaada wa mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wanaweza kujishonea taulo hizo na kujisitiri.

Private  Monica Constantino Nyagawa, analinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC chini ya bendera ya Umoja wa MAtaifa. Yeye anatoka Tanzania.
MONUSCO

Amani ni pamoja kuwapatia huduma za afya wananchi DRC- Mlinda amani TANZBATT_8  

Walinda amani wa Tanzania wanaohudumu katika kikosi cha 8, TANZBATT_8 kwenye Brigedi ya kujibu mashambulizi, FIB ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO wamezungumzia kile ambacho wanafanya katika kusongesha jukumu la Umoja wa Mataifa la kulinda amani kwenye taifa hilo lililogubikwa na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe kwa miongo kadhaa sasa.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiweka shada la maua kwenye hafla ya kuwaenzi na kuadhimisha siku ya walindamani duniani
UN Photo/Mark Garten)

UN yaenzi kujitolea na ujasiri wa walinda amani

Mchango wa vijana katika kuleta amani haupingiki na kuanzia Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR hadi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC mpaka Lebanon, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanafanya kazi na vijana kupunguza machafuko na kudumisha amani, ikiwemo upokonyaji wa silaha, kuwakusanya na kuwarejesha tena katika jamii na kuwaingiza katika program za kupunguza machafuko katika jamii.