Wakimbizi Hoima, Uganda, waishukuru UN kwa ulinzi mwaka 2021
Kuelekea mwaka mpya wa 2022 wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wanaoishi katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali wilaya ya Hoima nchini Uganda wametoa shukrani zao kwa Umoja wa Mataifa huku wakiomba usaidizi zaidi mwaka ujao wakati huu ambapo bado kuna changamoto za kimaisha zinazosababishwa na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19.