Kimsingi UNHCR haitakiwi iwepo iwapo tutatimiza wajibu wetu- Grandi
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) limetimiza miaka 70 tangu kuanzishwa kwake ambapo Kamishna Mkuu wa shirika hilo Filippo Grandi amesema “niondoeni kwenye jukumu hili” kwa kushughulikia visababishi vya mamilioni ya watu kukimbia makwao kutokanana vita na ukosefu wa usalama.