Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Wakimbizi wakiwa katika kituo cha afya kilichoko katika kambi yao ya Nakivale nchini Uganda
IRIN/Samuel Okiror

Mume wangu na wanangu 4 waliuawa napata faraja kwa kuwasaidia wanawake wengine:Sabuni Chikunda

Tukiwa bado na siku 16 za harakati za kupinga uakatili wa kijinsia dhidi ya wanawake, leo tunamulika mwanaharakati wa haki za binadamu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , Francoise Sabuni Chikunda ambaye amepitia madhila yasiyoelezeka, ikiwemo kubakwa na hata familia yake kuuawa, lakini yote hayo hayakumkatisha tamaa bali yamempa ujasiri wa kuwa nuru ya wanawake wakimbizi wenzake katika makazi ya wakimbizi ya Nakivale nchini Uganda.

Sauti
2'30"