Vita nchini DRC vinachochea njaa, ukatili wa kijinsia na watu kutawanywa: UN na wadau
Taarifa ya Wakuu wa Kamati ya Kudumu ya Mashirika ya Kimataifa kuhusu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC leo imeonya kwamba viwango vya juu vya machafuko nchini DRC vinachochea idadi kubwa ya watu kutawanywa, ukatili dhidi ya raia ambao hayajawahi kutokea na janga la njaa.