Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiweka shada la maua kwenye hafla ya kuwaenzi na kuadhimisha siku ya walindamani duniani
UN Photo/Mark Garten)

UN yaenzi kujitolea na ujasiri wa walinda amani

Mchango wa vijana katika kuleta amani haupingiki na kuanzia Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR hadi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC mpaka Lebanon, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanafanya kazi na vijana kupunguza machafuko na kudumisha amani, ikiwemo upokonyaji wa silaha, kuwakusanya na kuwarejesha tena katika jamii na kuwaingiza katika program za kupunguza machafuko katika jamii.

Mhudumu wa afya akimchanja dhidi ya Ebola, mwanaume mjini Beni, mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.
World Bank/Vincent Tremeau

Mlipuko wa 12 wa Ebola Kivu Kaskazini umetokomezwa - WHO 

Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO hii leo kupitia taarifa iliyotolewa mjini Brazzaville Congo na  Kinshasa, DRC, limetangaza kumalizika kwa mlipuko wa 12 wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, miezi mitatu tu baada ya mgonjwa wa kwanza kuripotiwa Kivu Kaskazini.