Mlinda amani kutoka Pakistani auawa DRC
Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC mlinda amani wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO, kutoka Pakistan ameuawa hii leo katika shambulio huko jimbo la Kivu Kusini.
Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC mlinda amani wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO, kutoka Pakistan ameuawa hii leo katika shambulio huko jimbo la Kivu Kusini.
Watu zaidi ya millioni moja , wakiwemo watoto 800,000 wamesambaratishwa na ghasia za kikabila pamoja na mapigano kati ya vikosi vya serikali,dhidi ya makundi yenye silaha na makundi ya wanamgambo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo yaani DRC
Nchini Tanzania shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi linahaha kusaidia hospitali ya Nyarugusu mkoani Kigoma ili iweze kuboresha huduma zake ili hatimaye kupunguza vifo vya watoto wachanga. Taarifa zaidi na Assumpta Massoi.
Katika Jarida la Umoja wa Mataifa hii leo tunaanzia huko DR Congo, ukiukwaji wa haki za binadamu wafurutu ada.
Nchini Uganda, milipuko ya homa ya Kongo na Bonde la Ufa yarejea.
Ukiukaji wa haki za binadamu uliongezeka kwa zaidi ya asilimia 25 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mwaka uliopita ikilinganishwa na mwaka uliotangulia, imesema ofisi ya pamoja ya haki za binadamu ya Umoja waMataifa nchini humo hii leo. Assumpta Massoi na ripoti kamili.
Kikosi cha jeshi la India kilichoko mkoa wa Malakal Sudan Kusini, kama sehemu ya kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa kimetoa msaada wakutibu mifugo ya wafugaji wa eneo la Akola,lililoko umbali wa kilomita sitini na tano, kaskazini mashariki mwa mji mkuu wa jimbo hilo.
Ili amani ya kweli na ya kudumu iweze kurejea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ni lazima wadau wote wa kisiasa ikiwemo serikali, chama tawala, wapinzani, asasi za kiraia na tume ya uchaguzi watimize wajibu wao katika kuhakikisha maandalizi ya uchaguzi mkuu yanaendelea kwa wakati kama ilivyopangwa.
Mkuu wa operesheni za ulinzi za Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix amewajulia hali walinda amani wawili wa Tanzania waliolazwa katika hospital ya Mulago mjini Kampala nchini Uganda.
Patrice Lumumba, Waziri Mkuu wa kwanza wa taifa huru la Congo, alihudumu kwa wiki kumi tu madarakani, lakini amesalia kuwa mtu mashuhuri na shujaa- kwa baadhi ya watu na kwa wengine jitu la kutisha!