DRC: Ukosefu wa usalama wafurusha takriban watu 530,000 jimboni Kivu Kaskazini - OCHA
Wakati zaidi ya Wananchi 7,000 raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC wamepata hifadhi katika nchi jirani ya Uganda, ofisi ya Umoja wa Mataifa ya uratibu wa misaada ya dharura OCHA imesema takriban watu 521,000 wameyakimbia makazi yao tangu Machi 2022 kutokana na mapigano katika maeneo ya Rutshuru na Nyiragongo, kaskazini mwa DRC.