Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Charlotte Fatuma, mkimbizi kutoka DRC anaendesha duka kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Coranne nchini Msumbiji kutokana na umeme ambao umefanikishwa na mradi unaotekelezwa na UNHCR, Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika.
UNHCR Video

Utu na maendeleo vyakutanishwa Coranne na kuleta ustawi kwa wakimbizi na wenyeji

Charlotte Fatuma na Neema Cenga ni wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na sasa wanaishi ukimbizini nchini Msumbiji katika jimbo la Nampula. Kwa sasa Charlotte ni mjasiriamali mwenye mafanikio makubwa, akiendesha biashara ya duka kwenye makazi ya wakimbizi ya Coranne huku Neema naye akijitahidi kulea na kusomesha watoto wake.  

Sauti
4'28"
Nyiranzaba na watoto wake tisa wanapata hifadhi kwenye hema baada ya kukimbia kijiji chake katika eneo la Rutshuru, jimbo la Kivu Kaskazini, DR Congo.
© UNICEF/Arlette Bashizi

Vurugu za sasa DRC ni ishara ya onyo - Mshauri Maalumu wa UN kuhusu kuzuia mauaji ya kimbari 

Kufuatia ziara yake rasmi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuanzia tarehe 10-13 Novemba 2022, Mshauri Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu kuzuia mauaji ya kimbari, Alice Wairimu Nderitu amesikitishwa sana na kuongezeka kwa ghasia katika Ukanda wa Maziwa Makuu ambako Mauaji ya Kimbari yam waka 1994 dhidi ya Watutsi nchini Rwanda yalitokea.