Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Vijana wanaharakati wa tabianchi huko Maldives wakipaza sauti zao wakihimiza hatua za kukuza mazingira zichukuliwe..
© UNICEF/Pun

Uzalishaji wa hewa chafuzi: Mataifa lazima yaende mbali zaidi kuliko ahadi za sasa - UNEP

Wakati joto la ulimwengu na uzalishaji wa hewa chafuzi vikivunja rekodi katika mwaka huu wa 2023, Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP) ya Pengo la Uzalishaji hewa chafuzi iliyotolewa leo Novemba 20 mjini Nairobi Kenya imeeleza kwamba imegundua kuwa ahadi za sasa chini ya Mkataba wa Paris zinaweka ulimwengu kwenye mstari wa ongezeko la joto la nyuzi joto 2.5 hadi 2.9 za Selsiasi zaidi ya viwango vya kabla ya kuanza kwa viwanda katika karne hii.

Sauti
2'12"
UN News/George Musubao

Umoja wa Mataifa unasimama na Afrika kutatua janga la tabianchi – Joyce Msuya

Ijumaa wiki ijayo yaani tarehe 24 vitaanzaa vikao vya awali kuelekea COP 28 ambao ni Mkutano wa  mabadiliko ya tabianchi utakaofanyika Dubai huko Falme za Kiarabu mwishoni mwa mwezi huu kuanzia tarehe 30.

Kuelekea mkutano huu, Naibu wa Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA, Joyce Msuya ameutumia mwezi huu kufanya ziara katika nchi nne za kusini na mashariki mwa Afrika ambako amesisitiza dhamira ya Umoja wa Mataifa ya kusimama na watu na Serikali za ukanda huo wakati janga la tabianchi linafanya mahitaji ya kibinadamu kuwa ya juu zaidi.

Sauti
1'33"
Mashambulizi ya makombora kutoka angani yamesababisha uharibifu mkubwa kwenye mji wa kusini wa Rafah ulioko Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israel
© UNICEF/Eyad El Baba

Habari kwa ufupi:

Mkutano wa kimataifa  kuhusu Gaza wafanyika jijini Paris Ufaransa, FAO inakabiliana na changamoto ya El Niño kwa wakulima na WHO kujenga mifumo ya afya yenye mnepo