Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Ripoti: Suluhu za asili zitumike kutatua changamoto za SDGs na Mabadiliko ya tabianchi
Suluhu za miundombinu ya asili zinaweza kuleta athiri chanya kwa asilimia 79 ya shabaha zote katika kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu- SDGs, hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na uhifadhi wa bioanuwai, imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Mapinduzi ya kijeshi Myanmar yamechochea hali mbaya ya haki na kibinadamu: Wataalamu UN
Wataalamu huru wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo wameonya kwamba mapinduzi ya kijeshi nchini Myanmar siyo tu kwamba yamesababisha mzozo wa haki za binadamu na masuala ya kibinadamu, bali pia yameongeza mazingira magumu ya mabadiliko ya tabianchi kwa watu wa Myanmar.
Uzalishaji wa hewa chafuzi: Mataifa lazima yaende mbali zaidi kuliko ahadi za sasa - UNEP
Wakati joto la ulimwengu na uzalishaji wa hewa chafuzi vikivunja rekodi katika mwaka huu wa 2023, Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP) ya Pengo la Uzalishaji hewa chafuzi iliyotolewa leo Novemba 20 mjini Nairobi Kenya imeeleza kwamba imegundua kuwa ahadi za sasa chini ya Mkataba wa Paris zinaweka ulimwengu kwenye mstari wa ongezeko la joto la nyuzi joto 2.5 hadi 2.9 za Selsiasi zaidi ya viwango vya kabla ya kuanza kwa viwanda katika karne hii.
Umoja wa Mataifa unasimama na Afrika kutatua janga la tabianchi – Joyce Msuya
Ijumaa wiki ijayo yaani tarehe 24 vitaanzaa vikao vya awali kuelekea COP 28 ambao ni Mkutano wa mabadiliko ya tabianchi utakaofanyika Dubai huko Falme za Kiarabu mwishoni mwa mwezi huu kuanzia tarehe 30.
Kuelekea mkutano huu, Naibu wa Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA, Joyce Msuya ameutumia mwezi huu kufanya ziara katika nchi nne za kusini na mashariki mwa Afrika ambako amesisitiza dhamira ya Umoja wa Mataifa ya kusimama na watu na Serikali za ukanda huo wakati janga la tabianchi linafanya mahitaji ya kibinadamu kuwa ya juu zaidi.
Janga la tabianchi Afrika: Umoja wa Mataifa unasimama na nyinyi - Joyce Msuya
Ijumaa wiki ijayo yaani tarehe 24 vitaanzaa vikao vya awali kuelekea COP 28 ambao ni Mkutano wa mabadiliko ya tabianchi utakaofanyika Dubai huko Falme za Kiarabu mwishoni mwa mwezi huu kuanzia tarehe 30.
Mazungumzo mapya kuhusu uchafuzi wa plastiki yanafanyika Nairobi: UNEP
Wanaharakati kutoka kote ulimwenguni wamekusanyika Nairobi, Kenya, kuanzia Jumatatu wiki hii kwa mazungumzo mapya juu ya mkataba wa kihistoria wa kimataifa wa kukabiliana na uchafuzi wa taka za plastiki.
Habari kwa ufupi:
Mkutano wa kimataifa kuhusu Gaza wafanyika jijini Paris Ufaransa, FAO inakabiliana na changamoto ya El Niño kwa wakulima na WHO kujenga mifumo ya afya yenye mnepo