Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Mwanafunzi Msumbiji: Iwe mvua iwe upepo mkali madarasa yetu ni salama
Kila mwaka, Msumbiji hukabiliwa na matukio ya hali mbaya za hewa kupindukia kama vile vimbunga na mafuriko, matukio ambayo husababisha uharibifu wa shule na hatimaye watoto kushindwa kujifunza. Hata hivyo, ujenzi wa madarasa yanayohimili matukio kama vile pepo kali na mafuriko umeleta nuru na matumiani kwa watoto, wazazi na walimu. Madarasa haya yanawezesha watoto kubakia salama hata wakati wa mvua na upepo mkali. Hali hii ni uwekezaji wa kudumu kwani ni hakikisho kwa watoto kuendelea kupata elimu na mustakabali wao kuwa bora.
Mwaka 2024 tishio kwa watoto: Ripoti ya UNICEF
Duniani kote mwaka 2024, watoto wanatarajiwa kuona kuongezeka kwa matukio ya ghasia, vita na matatizo ya kiuchumi, linasema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF), katika utafiti uliotolewa siku ya Jumatatu ya Januari 15, 2024.
Guterres: Vita, mabadiliko ya tabianchi na AI ni changamoto tunazopaswa kuzishughulikia haraka
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo amehutubia jukwaa la uchumi duniani mjini Davos Uswis akigusia changamoto mbalimbali zinazpoikabili dunia hivi sasa kuanzia vita inayoendelea Gaza na kwingineko, hali ya kutochukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na maendeleo ya akili mnemba au AI.
Jukwaa la kimataifa la wakimbizi lahitimishwa kwa ahadi ya dola bilioni 2.2 kuboresha maisha ya wakimbizi na jamii zinazowahifadhi: UNHCR
Jukwaa la kimataifa la wakimbizi GRF linalofanyika kila baada ya miaka minne ambalo ni mkusanyiko mkubwa zaidi duniani unaojadili masuala ya wakimbizi limekunja jamvi hii leo mjini Geneva Uswisi.
13 DESEMBA 2023
Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa COP28 ambao unafunga pazia leo. Pia tunamulika Kongamano la Kimataifa la Wakimbizi. Makala tunasalia huko huko Duabai kwenye mkutano wa COP28 na mashinani inamulika afya ya uzazi na haki za wanawake na wasichana walio katika mazingira magumu.
Wakimbizi vijana dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kambini Tongogara, Zimbabwe
Ikiwa leo Kongamano la Kimataifa la Wakimbizi ambalo hufanyika kila baada ya miaka minne linaanza huko Geneva, Uswisi na kuwaleta pamoja wadau mbalimbali wakiwemo wakimbizi kutafuta suluhu na kuahidi hatua kwa ajili ya wakimbizi duniani na nchi na jamii zinazowahifadhi, nikupeleke sasa nchini Zimbabwe ambako kuna mfano wa wazi namna wakimbizi wanavyoweza kuwa na mchango chanya katika jamii zinazowahifadhi.
UN: COP28 yafunga pazia kwa muafaka wa kuanza kutokomeza mafuta kisuskuku
Hatimaye mkutano wa 28 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP28, leo umekunja jamvi mjini Dubai huko Umoja w Falme za Kiarabu (UAE) kwa muafaka ambao Umoja wa Mataifa unasema unatoa ishara ya kuanza kutokomezwa kwa mafuta kisukuku au Fossil Fuels, ingawa baadhi ya nchi za visiwa vidogo vinavyoendelea ikiwemo Samoa zinaona muafaka huo hautoshelezi kuwalinda kikamilifu dhidi ya tabianchi.
UNICEF yafafanua ni kwa vipi mabadiliko ya tabianchi yanabebesha watoto mzigo wa magonjwa na ujinga.
Mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi hauathiri sayari dunia pekee bali pia unawabadilisha kabisa watoto. Watoto wanalazimika kubeba mzigo mkubwa wa magonjwa ya moyo, yale yanayosababishwa na matumizi ya maji machafu, yale yasababishwayo na kuvuta hewa chafu, pamoja na madhara ya kiakili na kihisia.
Muongo uliopita ndio ulikuwa na joto la kupindukia katika historia: WMO Ripoti
Muongo uliopita umethibitishwa kuwa na joto zaidi kuwahi kurekodiwa katika historia, na kuendeleza mwelekeo wa kutisha wa miaka 30 amesema leo mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO akiongeza kuwa hali hiyo imechochewa bila shaka na utoaji wa gesi chafuzi kutokana na shughuli za binadamu.