Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

05 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Assumpta Massoi 
-Lebanon,iko katika siku ya maombolezo kufuatia mlipuko mkubwa wa jana katika mji mkuu Beirut UNIFIL iko tayari kusaidia.
 - Nchini Niger, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linashirikiana na wadau kutekeleza mbinu za haraka za kukabiliana na utapiamlo uliokithiri miongoni mwa watoto .
- Takwimu za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR zinaonesha kuwa theluthi mbili ya raia milioni mbili wa Sudan Kusini wanaoishi uhamishoni, ni watoto.

-Na le

Sauti
11'52"
UN News

COVID-19 imeongeza chumvi katika kidonda changu cha athari za mabadiliko ya tabianchi-Jemima Hosea 

Kutokana na mwamko wa watu nchini Tanzania kuyapenda mazingira ya nyumba zao, Jemima Hosea wa jijini Dar es Salaam, aliona hiyo ni fursa ya yeye kujipatia kipato kwa kuotesha na kuuza maua ya aina mbalimbali. Katika kipindi ambacho biashara yake ilikuwa imeanza kushamiri ndipo likaibuka janga la virusi vya corona vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19. Janga hili likaongeza machungu katika changamoto aliyokuwa anapambana nayo mfanyabiashara huyu-changamoto ya mabadiliko ya tabianchi. Stella Vuzo wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa amemtembelea Jemima na kutuandalia makala hii. 

Sauti
2'49"
FAO/Rudolf Hahn

Uhusiano kati ya biashara yetu na mazingira ni wa ajabu sana-Wauza miche ya miti Tanzania

Biashara ya uuzaji wa miche ya miti nchini Tanzania hususani katika jiji la Dar es Salaam ni ya miaka mingi. Wauzaji wanasema ingawa uhusiano kati ya miti na mazingira ni  wa wazi mno, lakini kwao uhusiano huu ni wa ajabu. Wauza miti wanasema wanauza miti ili iende kuyatunza mazingira, na mazingira kwa haraka yanawalipa kwa kuwaletea mvua ambayo ni muhimu sana kwa biashara yao. Ungana na Ahimidiwe Olotu wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam aliyefunga safari hadi katika eneo la Mabibo, Ubungo Dar es Salaam kukutana na wafanyabiashara hawa. 

Audio Duration
3'30"

17 JUNI 2020

Katika Jarida la Habaroi hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Flora Nducha anakuletea

-  Bei ya chajo ya homa ya vichomi au  ‘Numonia’ imeshuka, na kuleta ahueni kwa nchi maskini umesema leo Umoja wa Mataifa

-Ikiwa leo ni siku ya kukabiliana na ongezeko la jangwa na ukame duniani Umoja wa Mataifa umeitaka dunia kuchukua hatua kulinda sayari tunayoishi kwani afya ya binadamu inategemea afya ya sayari hii

Sauti
9'58"
UNDP/Azza Aishath

COVID-19 inatupa fursa na wajibu wa kuimarisha uhusiano wetu na asili: Guterres

Ikiwa leo ni siku ya bahari duniani , Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema janga la virusi vya Corona au COVID-19 ni kumbusho kwamba binadamu wote wanahusiana wenyewe lakini pia na asili. Tupate ufafanuzi zaidi na Jason Nyakundi

Guterres ameyasema hayo kupitia ujumbe wake maalum wa siku hii ambayo kila mwaka huadhimishwa June 8 na kusistiza kwamba wakati dunia ikijitahidi kukomesha janga hili la COVID-19 na kujijenga upya ni fursa muhimu ya kubadilika

Sauti
1'56"
Niger inakumbana na upungufu wa chakula na viwango vya mapato ya chini
WFP/Simon Pierre Diouf

COVID-19 na mabadiliko ya tabianchi vyahitaji ujasiri na utashi kuvishinda:UN

Ili kukabiliana na janga la virusi vya corona au COVID-19 na tishio linguine linalonyemelea la mabadiliko ya tabianchi njia pekee ya kukabiliana nayo ni “ujasiri, maono na uongozi wa ushirikiano, ukijikita katika mshikamano wa kimataifa amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wakati wa majadiliano ya kimataifa hii leo yaliyojikita katika mabadiliko ya tabianchi.

UN News/Assumpta Massoi

Wananchi wanaelewa kuhusu mabadiliko ya tabianchi baada ya kuiona hali halisi

 Mafuriko, mvua za kupindukia, ukame na kuyeyuka kwa barafu ni ishara kubwa ya mabadiliko ya tabianchi lakini ni hadi wakazi wa ulimwengu wayashuhudie ndipo wanaamini, hivyo ndivyo anavyoeleza Kaimu Afisa Mazingira wa wilaya ya Pangani katika mahojiano na Saa Zumo wa Redio washirika Pangani FM, kuhusu hatua na harakati zinazofanywa na mamlaka ya wilaya ya Pangani katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

 
 
 
 
 
 
Sauti
2'19"