Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
05 Agosti 2020
-Na le
Moto na kuyeyuka kwa barafu Arctic vyahitaji hatua za haraka dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:WMO
Shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO leo limesema joto kali la kupindukia na la muda mrefu Siberia limesababisha sehemu ya Arctic kuwa na joto kuliko kawaida na kuchochea kuzuka kwa moto wa nyika kwa mwaka wa pili mfululizo huku likionya pia kuhusu kupungua kwa kasi kwa barafu baharini kwenye pwani ya Urusi.
COVID-19 imeongeza chumvi katika kidonda changu cha athari za mabadiliko ya tabianchi-Jemima Hosea
Kutokana na mwamko wa watu nchini Tanzania kuyapenda mazingira ya nyumba zao, Jemima Hosea wa jijini Dar es Salaam, aliona hiyo ni fursa ya yeye kujipatia kipato kwa kuotesha na kuuza maua ya aina mbalimbali. Katika kipindi ambacho biashara yake ilikuwa imeanza kushamiri ndipo likaibuka janga la virusi vya corona vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19. Janga hili likaongeza machungu katika changamoto aliyokuwa anapambana nayo mfanyabiashara huyu-changamoto ya mabadiliko ya tabianchi. Stella Vuzo wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa amemtembelea Jemima na kutuandalia makala hii.
Uhusiano kati ya biashara yetu na mazingira ni wa ajabu sana-Wauza miche ya miti Tanzania
Biashara ya uuzaji wa miche ya miti nchini Tanzania hususani katika jiji la Dar es Salaam ni ya miaka mingi. Wauzaji wanasema ingawa uhusiano kati ya miti na mazingira ni wa wazi mno, lakini kwao uhusiano huu ni wa ajabu. Wauza miti wanasema wanauza miti ili iende kuyatunza mazingira, na mazingira kwa haraka yanawalipa kwa kuwaletea mvua ambayo ni muhimu sana kwa biashara yao. Ungana na Ahimidiwe Olotu wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam aliyefunga safari hadi katika eneo la Mabibo, Ubungo Dar es Salaam kukutana na wafanyabiashara hawa.
17 JUNI 2020
Katika Jarida la Habaroi hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Flora Nducha anakuletea
- Bei ya chajo ya homa ya vichomi au ‘Numonia’ imeshuka, na kuleta ahueni kwa nchi maskini umesema leo Umoja wa Mataifa
-Ikiwa leo ni siku ya kukabiliana na ongezeko la jangwa na ukame duniani Umoja wa Mataifa umeitaka dunia kuchukua hatua kulinda sayari tunayoishi kwani afya ya binadamu inategemea afya ya sayari hii
Afya ya binadamu inategemea afya ya sayari tunayoishi:Guterres
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukabiliana na ongezeko la jangwa na ukame duniani Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameisihi dunia kulinda ardhi ya sayari tunayoishi kwani afya ya binadamu inategemea afya ya sayari hiyo.
COVID-19 inatupa fursa na wajibu wa kuimarisha uhusiano wetu na asili: Guterres
Ikiwa leo ni siku ya bahari duniani , Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema janga la virusi vya Corona au COVID-19 ni kumbusho kwamba binadamu wote wanahusiana wenyewe lakini pia na asili. Tupate ufafanuzi zaidi na Jason Nyakundi
Guterres ameyasema hayo kupitia ujumbe wake maalum wa siku hii ambayo kila mwaka huadhimishwa June 8 na kusistiza kwamba wakati dunia ikijitahidi kukomesha janga hili la COVID-19 na kujijenga upya ni fursa muhimu ya kubadilika
COVID-19 inatupa fursa na wajibu wa kuimarisha uhusiano wetu na asili: Guterres
Ikiwa leo ni siku ya bahari duniani , Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema janga la virusi vya Corona au COVID-19 ni kumbusho kwamba binadamu wote wanahusiana wenyewe lakini pia na asili.
COVID-19 na mabadiliko ya tabianchi vyahitaji ujasiri na utashi kuvishinda:UN
Ili kukabiliana na janga la virusi vya corona au COVID-19 na tishio linguine linalonyemelea la mabadiliko ya tabianchi njia pekee ya kukabiliana nayo ni “ujasiri, maono na uongozi wa ushirikiano, ukijikita katika mshikamano wa kimataifa amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wakati wa majadiliano ya kimataifa hii leo yaliyojikita katika mabadiliko ya tabianchi.
Wananchi wanaelewa kuhusu mabadiliko ya tabianchi baada ya kuiona hali halisi
Mafuriko, mvua za kupindukia, ukame na kuyeyuka kwa barafu ni ishara kubwa ya mabadiliko ya tabianchi lakini ni hadi wakazi wa ulimwengu wayashuhudie ndipo wanaamini, hivyo ndivyo anavyoeleza Kaimu Afisa Mazingira wa wilaya ya Pangani katika mahojiano na Saa Zumo wa Redio washirika Pangani FM, kuhusu hatua na harakati zinazofanywa na mamlaka ya wilaya ya Pangani katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi.