Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
WFP yasema mabadiliko ya tabianchi yanaleta changamoto kubwa kwa wanawake wavuvi Ecuador:WFP
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP limesema mabadiliko ya tabianchi ni changamoto kubwa nchini Ecuador hasa kwa wanawake wanaotegemea na kufanya kazi ya uvuvi.
14 JANUARI 2020
Katika Jarida la Habari hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Grace Kaneiya anakuletea
-Dola milioni 477 zahitajika ili kunusuru maisha ya takriban watu laki tisa nchini Sudan kwa mahitaji ya kibinadamu kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR lililozindua ombi hilo leo mjini Khartoum
-Ofisi ya miradi ya Umoja wa Mataifa, UNOPS kwa kushirikiana na Benki ya dunia pamoja na wadau wenyeji, wanafanya juhudi za kuboresha huduma mijini pamoja na nishati ya umeme kwa mamilioni ya watu wa Yemen.
Mabadiliko ya tabianchi yanaleta changamoto kubwa kwa wanawake wavuvi Ecuador:WFP
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP limesema mabadiliko ya tabianchi ni changamoto kubwa nchini Ecuador hasa kwa wanawake wanaotegemea na kufanya kazi ya uvuvi.
Je wajua kuwa ukubwa wa ziwa Tanganyika unazidi kupungua?
Nchini Tanzania, Ziwa Tanganyika lililopo mkoani Kigoma lasifika kwa kuwa la pili kwa kuwa na kina kikubwa zaidi duniani. Hata hivyo, kina na ukubwa wa ziwa vinapungua kutokana na mabadiliko ya tabianchi na shughuli za binadamu. Miongoni mwa mashuhuda wa hali hiyo ni Bwana Kassim Govola Mbingo ambaye ni mhifadhi mkuu katika makumbusho ya Dkt. David Livingstone mjini Ujiji mkoani Kigoma. Katika mahojiano yake na Assumpta Massoi wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa anafafanua
13 JANUARI 2020
Katika Jarida la Habari hii leo Grace Kaneiya anakuletea
-Miaka 10 baada ya tetemeko baya la ardhi nchini Haiti athari zake zinaendelea kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM
-Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeutenga mwaka 2020 kuwa ni wa afya ya mimea kwa kutambua mchango na thamani ya mimea hiyo kwa maisha ya watu na syari dunia
-Maelfu ya Wavenezuela wakiwemo watoto wanaendelea kufungasha virago na kukimbilia nchi jirani ikiwemo Brazil limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF
Mwaka 2020 ni mwaka wa afya ya mimea ambayo mara nyingi hupuuzwa-UNEP/FAO
Mashirika ya Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira duniani UNEP, na la chakula na kilimo FAO yamesema mimea ndio kila kitu katika kuhakikisha uhai wa mamilioni ya watu duniani na sayari tunayoishi, lakini cha kusikitisha ni kwamba mara nyingi mimea hiyo haipewi uzito unaostahili.
Nchini Burkina Faso mradi wa FAO wa kukabiliana na jangwa wazaa matunda
Mradi wa kimataifa wa kukabiliana na jangwa ulioashindwa na shitrika la Umoja wa Mataifa la chakula la kilimo FAO umeanza kuleta nuru kwa wakulima nchini Burkina Faso
09 JANUARI 2020
Katika Jarida letu la Habari hii leo Arnold Kayanda anakuletea
-UNHCR yatoa changamoto kwa Muungano wa Ulaya kuufanya mwaka 2020 kuwa wa ulinzi kwa wakimbizi na wahamiaji
-Kuanza tena kwa doria inayojumuisha mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Mali MINUSCA ni neema na amani kwa raia
-Nchini Burkina Fasso mradi wa pamoja wa shirika la chakula na kilimo FAO, Muungano wa afrika Au na serikali ya nchi hiyo kupambana na hali ya jangwa umeleta tija kwa wananchi
-Makala yetu hii leo inatupeleka Uganfa kumulika ugonjwa wa ukimwi , wakimbizi na sekta ya mafuta
Mradi wa FAO wa kukabiliana na jangwa wazaa matunda Burkina Faso
Mradi wa kimataifa wa kukabiliana na jangwa ulioashindwa na shitrika la Umoja wa Mataifa la chakula la kilimo FAO umeanza kuleta nuru kwa wakulima nchini Burkina Faso
Sitisheni uhasama, dunia inashuhudia migogoro zaidi katika karne hii-Antonio Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres leo Jumatatu amesema migogoro ya mataifa inachangia katika nchi nyingi zaidi kuchukua uamuzi ambao matokeo yake hayatabiriki na yanazua hatari kubwa ya matokeo ya mipango mibovu.