Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

26 Oktoba 2021

26 Oktoba 2021

Pakua

Karibu usikilize jarida ambapo leo Assumpta Massoi amekuandalia habari mbalimbali zikiwemo

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP imeeleza kuwa ahadi mpya na zilizorekebishwa kuhusu viwango vya nchi vya kukabili mabadiliko ya tabianchi, NDCs hazijafikia lengo lililowekwa katika mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi na hivyo ulimwenguni kuwa hatarini kuwa na ongezeko la joto la angalau nyuzijoto angalau 2.7 katika karne hii.

Pamoja na rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema wameomba mazungumzo na mashirika ya Umoja wa Mataifa ikiwemo UNHCR kusaidia nchi ambako wakimbizi wanatoka ili waweze kurejea akitolea mfano Burundi.

 

 

Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
11'59"