Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
05 Novemba 2021
Karibu kusikiliza jarida ambapo leo ni siku ya kimataifa ya uelimishaji kuhusu Tsunami, na kama ilivyo ada leo ni mada kwa kina ambapo tunaangazia vijana na mchango wao katika mabadiliko ya tabianchi wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa COP26 ukiendelea huko Glasgow Scotland.
Flora Nducha amezungumza na mmoja wa vijana wanaharakati wa mazingira kutoka nchini Kenya na mshindi wa tuzo ya shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP ya champion of the Earth 2020 kutokana na kampuni yake ya Change Makers kubadili taka za platiki kuwa tofali.
Vijana tunaweza ni wakati wa kutushirikisha kwa vitendo katika vita dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:Nzambi
Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26 ukiendelea mjini Glasgow Scotland, vijana wanatoa wito kwa viongozi kutekeleza kwa vitendo ushirikishwaji wa vijana katika vita dhidi ya janga hilo.
Mauritania wapambana na mabadiliko ya tabianchi
siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano huo wa 26 wa nchi wanachama wa mabadiliko ya tabianchi, ambao hivi sasa unaendelea Glascow, Scotland, Mshauri Maalumu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudunia wakimbizi, UNHCR kuhusu Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi, Andrew Harper ametembelea Mauritania kujionea jinsi wakimbizi wanavyopambana na janga la tabianchi.
(Taarifa ya John Kibego)
“Hatujawahi kuona mwaka kama 2021. Huu ni mwaka wenye mioto mingi ya nyika.” Anasema Ahmedou El-Bokhary, Rais wa Kikosi cha zima moto kinachoundwa na wakimbizi.
Ukame wasababisha wanakijiji kula dungusi kakati nchini Madagascar
Wakati mkutano wa mabadiliko ya tabianchi ungali ukiendelea huko Glasgow, Scotland, ukame unazidi kushika kasi kusini mwa Madagascar na watu wakiingia mwaka wa tano bila ya mvua hali inayowalazimu wananchi kula dungusi kakati kwa kuwa ndio mmea pekee unaoota kwenye maeneo yao.
04 Novemba 2021
Karibu kusikiliza jarida, leo ni siku ya kimataifa ya kupinga uonevu shuleni na mitandaoni ambapo UNESCO imetaka watoto kulindwa zaidi, WFP imetoa msaada kwa wananchi wa Madagascar wanaoishi katika ukame na hivyo kulazimika kula mmea wa Dungusi kakati.
Pia utasikia kauli ya Rais wa COP26 huko Glasgow kuhusu nchi tajiri kutoa fedha za kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
3 Novemba 2021
Karibu katika jarida ambapo utasikia kuhusu ushindi wa kijana mtanzania katika tuzo zilizotolewa leo sanjari na mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP26.
Habari kwa ufupi leo zimeangazia ripoti ya uchuguzi wa masuala ya haki za binadamu huko Tigray nchini Ethiopia na baa la njaa nchiniMadagascar
Zaidi ya nchi 100 zimeahidi kusitisha na kubadilisha ukataji miti ifikapo 2030
Azimio la kihistoria la kuokoa na kurejesha misitu ya dunia katika ubora wake limetangazwa leo rasmi katika siku ya pili ya mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi unaoshirikisha viongozi wa dunia au COP26.
Jamii ya Watyaba kandoni mwa Ziwa Albert nchini Uganda yatishiwa tena na mafuriko
Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26 unaendelea katika huko Glosgow na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiwa amewaeleza viongozi wa ulimwengu kuwa ni muhimu kuchukua hatua sasa kwani wanadamu wanajichimbia kaburi, nchini Uganda jamii ya Watyaba, mojawapo ya jamii za walio wachache wanaoishi katika viunga vya Ziwa Albert, wanapaza sauti kwa serikali na shirIka la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kuwasaidia kutokana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi.
02 Novemba 2021
Leo tarehe 02 Novemba 2021 siku ya kimataifa ya kutokomeza ukwepaji sheria kwa uhalifu dhidi ya wanahabari ASSUMPTA MASSOI anakuletea jaridi likizungumzia kwa undani juu ya siku hii na takwimu zilizotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni, UNESCO pamoja na ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
COP26: Jamii ndogo zina mchango mkubwa katika vita dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:Rahma Kivugo
Jamii ndogo ndogo za mashinani zina mchango mkubwa katika kusongesha ajenda ya Umoja wa Mataifa ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi amesema mmoja wa wanaharakatio wa mazingira Rahma Rashid Kivugo mratibu wa mradi wa kijamii wa Mikoko Pamoja kutoka Pwani ya Kenya.