Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mukhtasari wa Mkutano Mkuu kusailia uharibifu wa hewa duniani

Mkutano wa 12 kwa Mataifa 189 Yalioridhia Mkataba wa Hifadhi Dhidi ya Uharibifu wa Mabadiliko ya Hali ya Hewa pamoja na kuidhinisha Mkataba wa Kyoto ulianzishwa rasmi mwanzo wa juma mjini Nairobi, Kenya ambapo kulizingatiwa hatua za kudhibiti kipamoja athari za mabadiliko yaliyoletwa na uchafuzi wa hewa duniani.

Mahakama ya ICC yasikiliza kesi yake ya kwanza mjini Hague

Mahakama pekee ya kudumu ya kimataifa juu ya makosa ya jinai ya vita, yaani Mahakama ya ICC ilisikiliza kesi yake ya mwanzo Alkhamisi, Novemba tisa(2006), iliofanyika mjini Hague, Uholanzi inayohusika na Thomas Lubanga Dyilo, aliyekuwa jemadari wa kundi la wanamgambo wa kundi la Forces Patriotiques pour la Liberation du Congo (FPLC) katika wilaya ya Ituri, Mashariki-kaskazini ya JKK katika miaka ya 2002-03.