Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahakama ya ICC yasikiliza kesi yake ya kwanza mjini Hague

Mahakama ya ICC yasikiliza kesi yake ya kwanza mjini Hague

Mahakama pekee ya kudumu ya kimataifa juu ya makosa ya jinai ya vita, yaani Mahakama ya ICC ilisikiliza kesi yake ya mwanzo Alkhamisi, Novemba tisa(2006), iliofanyika mjini Hague, Uholanzi inayohusika na Thomas Lubanga Dyilo, aliyekuwa jemadari wa kundi la wanamgambo wa kundi la Forces Patriotiques pour la Liberation du Congo (FPLC) katika wilaya ya Ituri, Mashariki-kaskazini ya JKK katika miaka ya 2002-03.