Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mpango wa Utendaji wa UM Kudhibiti Silaha Ndogo Ndogo Wafanyiwa Mapitio

Miaka mitano baada ya Umoja wa Mataifa (UM) kupitisha Mpango wa Utendaji wa kukabiliana na biashara haramu ya silaha ndogo ndogo na silaha nyepesi katika dunia, Makao Makuu ya UM yalishuhudia mkusanyiko wa hali ya juu wa wawakilishi karibu 2,000 wa kimataifa kutoka serikali wanachama mbalimbali, pamoja na mashirika ya kikanda na kimataifa kwa makusudio ya kuzingatia uwezekano wa kulikomesha tatizo la kuenea kwa silaha ndogo ndogo na silaha nyepesi katika ulimwengu.

Risala ya nasaha ya Katibu Mkuu kwa Umoja wa Afrika(AU).

Katibu Mkuu (KM) wa Umoja wa Mataifa (UM) Kofi Annan kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Afrika (AU)uliofanyika majuzi katika mji mkuu wa Banjul, Gambia aliwaambia wajumbe wa Mataifa Wanachama ya kuwa anajumuika kusherehekea nao, kidhati, mafanikio ya kidemokrasia yaliyojiri miaka ya karibuni katika bara la Afrika.

Mkutano wa UM juu ya Tatizo la Silaha Ndogo Ndogo Duniani.

Mnamo mwaka 2001 wawakilishi wa Mataifa Wanachama katika UM walipitisha, kwa kauli moja, Mpango wa Utendaji uliokusudiwa kuihamasisha jamii ya kimataifa kushirikiana kuratibu kanuni mpya za kuboresha sheria za kitaifa zinazohitajika kudhibiti biashara haramu ya silaha ndogo ndogo ulimwenguni.