Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Chuo Kikuu cha Pretoria kutunukiwa zawadi ya UNESCO

Kitivo cha Haki za Kiutu cha Chuo Kikuu cha Pretoria, Afrika Kusini kinachosimamia mafunzo yanayohusu taratibu za kuimarisha haki za kimsingi kimetunukiwa zawadi ya dola 10,000 na Shirika la Umoja wa Mataifa juu ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Juhudi za Baraza Kuu kudhibiti biashara haramu ya almasi.

Mnamo mwanzo wa wiki Baraza Kuu la UM lilipitisha azimio la kuunga mkono Mpango wa Kimberley na kupendekeza utaratibu huo uendelea kuimarishwa kimataifa. Kabla ya azimio kupitishwa Mataifa Wanachama 192 wa UM walisikia ripoti ya mapitio kutoka Raisi Festus Gontebanye Mogae wa Botswana, Mwenyekiti wa mwaka huu wa nchi zilizoridhia na kuidhinisha Mpango wa Kimberley.

UM kupunguza wahudumia misaada ya kiutu katika Chad

UM umetangaza kwamba kutokana na hali ya usalama inayoendelea kuharibika katika eneo la Chad ya mashariki zile huduma za kupeleka misaada ya kihali kwa wahamiaji wa Sudan 110,000 waliopo huko zitabidi zipunguzwe pamoja na kupunguza wafanyakazi wa UM wanaohusika na kadhia hizo.