Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Balozi wa Kenya azingatia mkataba mpya dhidi ya silaha ndogo ndogo

Mwakilishi wa Kudumu wa Kenya katika UM, Balozi Zachary Muburi-Muita alifanya mahojiano na Redio ya UM ambapo alizungumzia, na kuzingatia yale mapendekezo ya baadhi ya wanadiplomasiya wa kimataifa - akiwemo pia Kamishna Mkuu Mstaafu wa Haki za Binadamu, Mary Robinson - ya kuanzisha kampeni ya kubuni chombo kipya cha sheria ya kimataifa ili kudhibiti bora biashara ya silaha ndogo ndogo ulimwenguni.

UNHCR itapanua operesheni zake Darfur Magharibi

Antonio Guterres, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) baada ya kumaliza ziara muhimu katika kambi za wahamiaji wa ndani ya nchi (IDPs), katika Sudan wiki hii, aliripoti kuwa amefikia maafikiano, na Serekali ya Sudan, yanayoruhusu kupanuliwa shughuli za UNHCR katika eneo la Darfur Magharibi.

Naibu KM azuru DRC kuimarisha amani

Naibu KM Asha-Rose Migiro wiki hii alifanya ziara ya siku tatu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC). Alipokuwepo huko alikutana kwa mazungumzo, na pia mashauriano, na Raisi Joseph Kabila pamoja na viongozi kadha wengine wa kisiasa, wakijumuisha vile vile wanasiasa wa kutoka vyama vya upinzani.

Hapa na pale

KM Ban Ki-moon aliwanasihi wajumbe wa kimataifa waliohudhuria Kikao cha Saba juu ua Demokrasia, Maendeleo na Biashara Huru, kilichofanyika Doha, Qatar kuhakikisha duru yao ya mazungumzo itawasilisha mafanikio ya kuridhisha, maana bila ya kuyafannya hayo, alionya, nchi masikini zitaporomoka zaidi kimaendeleo, hali ambayo anaamini itafumsha mitafaruku na kueneza hali ya wasiwasi kwenye mfumo mzima wa biashara katika soko la kimataifa.~

Mkataba wa Haki za Watu Walemavu Duniani Kuridhiwa Kimataifa (Sehemu ya Kwanza)

Mnamo mwisho wa mwezi Machi, Mataifa Wanachama 81 pamoja na Umoja wa Ulaya (EU) walijumuika kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa (UM) kutia sahihi mkataba mpya wa kihistoria, uliokusudiwa kuboresha maisha ya watu milioni 650 walemavu duniani na kuwatekelezea haki zao za kimsingi kama inavyostahiki. Mkataba huu, kwa ujumla, unakataza na kupiga marufuku, ubaguzi wa aina yoyote, katika sehemu zote za jamii dhidi ya watu walemavu.

Sudan imekubali furushi la ulinzi wa amani kwa Darfur

Serekali ya Sudan wiki hii ilituma barua kwa Baraza la Usalama ilioelezea kukubali kupelekwa katika Darfur helikopta zitakazotumiwa na vikosi vya mseto vya AU na UM katika shughuli za kuimarisha usalama na amani kwa raia wa jimbo la magharibi la Sudan la Darfur.

UNMIS kulaani mauaji ya ofisa wa jeshi la AU Darfur

Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani Sudan (UNMIS) limetoa taarifa yenye kulaani vikali mauaji ya ofisa wa Vikosi vya Amani vya Umoja wa Afrika (AMIS) yalioendelezwa na makundi ya watu wasiojulikana, mnamo tarehe 14 Aprili, kwenye kambi ya wanajeshi iliopo ElFasher.