Balozi wa Kenya azingatia mkataba mpya dhidi ya silaha ndogo ndogo
Mwakilishi wa Kudumu wa Kenya katika UM, Balozi Zachary Muburi-Muita alifanya mahojiano na Redio ya UM ambapo alizungumzia, na kuzingatia yale mapendekezo ya baadhi ya wanadiplomasiya wa kimataifa - akiwemo pia Kamishna Mkuu Mstaafu wa Haki za Binadamu, Mary Robinson - ya kuanzisha kampeni ya kubuni chombo kipya cha sheria ya kimataifa ili kudhibiti bora biashara ya silaha ndogo ndogo ulimwenguni.