Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Usalama laarifiwa na H. Annabi ratiba ya vikosi vya mseto kwa Darfur

Baraza la Usalama laarifiwa na H. Annabi ratiba ya vikosi vya mseto kwa Darfur

Wiki hii Baraza la Usalama lilikutana kwenye kikao cha faragha kusikiliza ripoti ya Hedi Annabi, Naibu Mkuu wa Idara ya UM juu ya Operesheni za Amani ambaye alielezea kuhusu ratiba ya siku zijazo inayotakikana kutekelezwa ili kuharakisha upelekaji wa kile kinachojulikana kama ‘furushi zito’ la vikosi vya mseto vya UM na AU katika Jimbo la Darfur, Sudan. Annabi alisisitiza kwenye risala yake juu ya jukumu adhimu la jumuiya ya kimataifa kuikamilisha kadhia hiyo ya amani kidharura.