Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Umoja wa Mataifa kufufua utaratibu wa amani Darfur

Umoja wa Mataifa kufufua utaratibu wa amani Darfur

Mjumbe maalum wa UM aliyepewa jukumu la kufufua utaratibu wa amani katika jimbo lenye ghasia la Darfur huko Sudan amewasili Sudan wiki hii kuanza mazungumzo mepya .

Jan Eliasson mjumbe maalum wa katibu mkuu kwa ajili ya Darfur alikutana na tume ya pamoja ya upatanishi ya Jumwia ya Afrika na UM mjini Khartoum, kujadili matayarisho ya mkutano wa pamoja wa kimataifa juu ya utaratibu wa kisiasa huko Libya. Mkutano huo utakao fanyika mjini Tripoli, tarehe 15 na 16 Julai utatathmini maendeleo yaliyopatikana mnamo miezi ya hivi karibuni kuitisha mkutano wa amani kwa ajili ya Darfur ambako zaidi ya watu laki mbili wameuwawa tangu kuanza ghasia 2003. Bw Eliasson alielekea magharibi ya Darfur kwa mazungumzo na vyama vya kisiasa makundi yasiyo ya kiserekali wajumbe wa watu walokimbia makazi yao na maafisa wa jimbo wanaohusika na utaratibu wa majadiliano.