Afghanistan itaendelea kuhitaji msaada wa kimataifa
Afghanistan inahitaji msaada wa kimataifa unaoendelea kama kweli inataka kuchukua majukumu ya nchi hiyo Machi 21 amesema balozi wa Afghanistan kwenye Umoja wa Mataifa Zahir Tanin.
Afghanistan inahitaji msaada wa kimataifa unaoendelea kama kweli inataka kuchukua majukumu ya nchi hiyo Machi 21 amesema balozi wa Afghanistan kwenye Umoja wa Mataifa Zahir Tanin.
Umoja wa Mataifa umewataka wagombea wa uchaguzi nchini Haiti hususan wa kiti cha Urais kuacha kutoa matamshi ya kushambulia pamoja na vitisho huku ghasia zinazoambatana na kampeni zikiendelea kabla ya kuandaliwa kwa uchaguzi siku ya Jumapili.
Afisa wa ngazi ya juu kwenye Umoja wa Mataifa amesema kuwa hata baada ya nchi ya Liberia kupiga hatua muhimu bado inahitaji kupewa uungwaji mkono wa kiamatifa wakati inapojiandaa kufanya uchaguzi na inapokabiliana na idadi kubwa ya wakimbizi kutoka Ivory Coast.
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na mpango wa chakula WFP imemwidhinisha mtangazaji wa zamani kutoka Canada George Stroumboulopoulos kuwa balozi wake wa masuala ya njaa.
UM yataka kuwepo juhudi zaidi kutokomeza vitendo vya ubakaji mpakani wa DRC na
Angola.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amejadili na viongozi wa amerika ya Kati kuhusu hali inayoendelea katika ulimwengu wa Kiarabu na Afrika ya Kaskazini hususan Libya.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili James Anaya ametoa wito wa mawasiliano zaidi baina ya serikali, watu wa asili na makabila huko Surinam na kuahidi kuendelea kusaidia juhudi za haki za watu hao za kumiliki ardhi na rasilimali zingine.
Wadau muhimu wanaojihusisha na masuala ya HIV na ukimwi wamekubaliana njia muafaka ya kusaidia kutokomeza maambukizi ya HIV kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa leo limeendelea na mjadala kuhusu azimio la kuiwekea vikwazo Libya.
Majeshi ya usalama nchini Bahrain yameteka kwa nguvu hospitali kadhaa na vituo vya afya kwa mujibu wa ofosi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa.