Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Juhudi kutokomeza ubakaji mpkani mwa DRC na Angola ziongezwe

Juhudi kutokomeza ubakaji mpkani mwa DRC na Angola ziongezwe

UM yataka kuwepo juhudi zaidi kutokomeza vitendo vya ubakaji mpakani wa DRC na

Angola.

Huku kukiwa na ripoti za kufanyika kwa vitendo vya ubakaji kwa mamia ya wanawake  ambao walikumbwa na vitendo hivyo wakati wakiwa njiani kurejea nyumba DRC toka  Angola afisa wa ngazi za juu wa umoja wa mataifa anayehusika na matukio ya  ubakaji kwenye maeneo yenye mizozo ametaka mamlaka za nchi zote mbili kuchunguza  madai hayo na wakati huo huo kuchukua hatua za haraka kuzua kutotokea tena kwa

vitendo hivyo.

Mkuu huyo Margot Wallstrom amezitolea mwito mamlaka za pande zote mbili  kuhakikisha zinawajibika kuwalinda na kuyatetea makundi ya kina mama ambayo mara  kwa mara yanatumbukia mikononi mwa makundi ya kihalifu. Ripoti za hivi karibuni zinasema kuwa zaidi ya watu 12,000 raia wa Jamhuri ya  Congo ambao walifukuzwa kutoka Angola kati ya Septemba na disemba mwaka uliopita  wanadaiwa kwamba walikumbwa na matukio ya ubakaji.

Timu ya waangalizi wanaohusika na misaada ya usamaria mwema walipotembelea  maeneo waliofikia wananchi hao wlaishuhudia matukio kadhaa ya kukatiza tama  pamoja na kuwepo kwa vitendo vya unyanyasaji kijisnia. Mwezi uliopita Bi Margot alikutana na waathirika hao na kisha kufanya nao majadiliano na baadaye alielekea nchini Angola ambako alikutana na maafisa wa  serikali