Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na Pale

KM ametoa taarifa maalumu, kwa kupitia msemaji wake, iliolaani vikali vitendo vya ukatili wa kukirihisha, ulioripotiwa kufanywa majuzi na waasi wa kundi la LRA katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK) na sehemu za Sudan Kusini. KM amesisitiza wafuasi wa LRA wanalazimika kuhishimu na kufuata

Hapa na Pale

Karen Abu Zayd, Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linalofarajia Misaada ya kwa Wahamiaji wa KiFalastina katika Mashariki ya Karibu (UNRWA), pamoja na Robert Serry, Mratibu Maalumu wa UM juu ya Mpango wa Amani Mashariki ya Kati (UNSCO) wamemtumia Waziri wa Ulinzi wa Israel, Ehud Barak, barua ya dharura, ya pamoja, yenye malalamiko makali dhidi ya matukio mawili ya “kushtusha” katika Tarafa ya Ghaza kuhusu usalama wa wafanyakazi wa UM na majengo yao, na barua iliomba Serikali ya Israel iipatie UM maelezo ya waziwazi juu ya matukio hayo.~

Baraza la Usalama lahimiza uhasama na vurugu usitishwe Ghaza

Baada ya majadiliano ya karibu saa tano, kwenye kikao cha dharura, wajumbe wa Baraza la Usalama waliokutana Ijumapili, alfajiri, waliafikiana kutoa taarifa maalumu kwa waandishi habari kuhusu hali ya vurugu lilioripuka Ijumamosi katika Tarafa ya Ghaza, eneo la Wafalastina liliokaliwa kimabavu .

Uchina yapeleka manowari mbili mwambao wa Usomali kupambana na maharamia

Imeripotiwa leo hii kwamba manowari mbili za Serikali ya Jamhuri ya Watu wa Uchina, pamoja na meli moja iliobeba shehena za kukidhi mahitaji ya wanamaji, zimeanza safari ya kuelekea kwenye eneo la mwambao wa Usomali kujiunga na manowari za mataifa mengine wanachama wa UM, kwa madhumuni ya kukabiliana na maharamia waliopamba karibuni katika sehemu hiyo ya Pembe ya Afrika.

Tetesi za Al-Jazeera juu ya UNMIS na ICC hazina msingi, inasema UM

Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani Sudan Kusini (UNMIS) imetoa taarifa yenye kukanya tetesi zilizochapishwa kwenye magazeti ya Khartoum, yakinakili shirika la habari la Al-Jazeera ambalo lilidai Mjumbe Maalumu wa KM kwa Sudan, na Mkuu wa UNMIS, Ashraf Qazi, alibashiria tarehe ya uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa juu ya Makosa ya Jinai ya Halaiki (ICC) kuhusu maombi ya kushikwa Ahmed Harun, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani wa Sudan na ambaye sasa ni Waziri wa Nchi juu ya Masuala ya Kiutu, pamoja na Ali Kushayb, kiongozi wa jeshi la mgambo la Janjaweed.