Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashirika ya UM yameanzisha kampeni ya kunusuru maisha kwa watoto wachanga na wanawake Usomali

Mashirika ya UM yameanzisha kampeni ya kunusuru maisha kwa watoto wachanga na wanawake Usomali

Mashirika ya UM juu ya afya duniani, WHO, na huduma za maendeleo ya watoto, UNICEF, yameanzisha kampeni ya kuchangisha mamilioni ya dola zitakazotumiwa kwenye miradi ya kunusuru maisha ya watoto milioni 1.5, walio chini ya umri wa miaka mitano katika Usomali, pamoja na kuwasaidia wanawake wa umri wa kuweza kuzaa, yaani baina ya miaka 15 hadi 49, kujidhibiti kiafya.