Sauti za wanakijiji zasailia Mradi wa Milenia Mbola
Katika makala zilizopita tulieleza kwamba Mbola ilikuwa ni moja ya vijiji vya Milenia viliopo Afrika kusini mwa Sahara, vilivyochaguliwa na UM kufanywa vijiji vya mfano, ambavyo uzoefu wake ulitarajiwa kutumiwa kuongoza udhibiti bora wa miradi ya MDGs katika sehemu nyengine za taifa, na pia katika Afrika, kwa ujumla. Tangu Miradi ya Milenia ilipoanzishwa hadi leo huduma kadha wa kadha ziliekezwa Kijijini Mbola, Tanzania, hususan katika sekta za kilimo, elimu, miundo mbinu, afya na kadhalika, shughuli ambazo zilionekana kushika mizizi ya kutia moyo katika kukabiliana na matatizo ya umasikini, na katika huduma za kuwapatia wanakijiji wa Mbola natija za kuwanyanyua kimaisha.