Sarah: Mjane shujaa anayeng'ara kupitia ufugaji nyuki
- Kutoka maombolezoni hadi mafanikioni
- Ufuaji wa nyuki waboresha maisha
- Mafunzo kutoka FAO yameimarisha vikundi na wanavikundi
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametumia maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela leo Julai 18 kutoa wito kwa mataifa na wananchi duniani kote kuimarisha juhudi za kupambana na umaskini, ukosefu wa usawa na ubaguzi wa kijamii, huku akiihimiza dunia kuendeleza maono ya kiongozi huyo mashuhuri wa Afrika Kusini.
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasiaya Congo, DRC, shirika la kiraia la Congo Notre Avenir, yaani kwa kiswahili, Congo Mustakabali wetu linapigania haki ya amani kwa wanawake ili hatimaye waweze kushiriki katika kuendeleza familia zao kwa kushirikiana na familia zao, wakati huu ambapo mapigano mashariki mwa nchi yamesababisha ukatili ikiwemo ubakaji, na hata wanaume kuacha familia zao na kwenda msituni kupigana.
Mifumo ya tahadhari za mapema dhidi ya majanga yanayosababishwa na mabadiliko ya tabianchi haitakuwa na manufaa ikiwa ujumbe hautawafikia watu kwa lugha wanazoelewa na kupitia njia wanazoziamini.
Je wewe ni mmoja wa watu ambao bila ushauri wa daktari unatumia virutubisho vya mafuta, vitamini na madini kwa lengo la kuimarisha mwili? Sasa makala hii inakuhusu kwani matumizi holela yanaonekana kuwa miongoni mwa visababishi vya ugonjwa wa kusahau. Bofya hapa kufahamu zaidi kuhusu ugonjwa huu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano wa kimataifa ili kuhakikisha kuwa akili mnemba (AI) inakuwa chachu ya maendeleo endelevu badala ya kuongeza pengo la ukosefu wa usawa duniani. Amesema teknolojia hiyo lazima iwahudumie watu, si watu kuitumikia teknolojia.
Mashirika mawili ya Umoja Umoja wa Mataifa lile la Uhamiaji, IOM na la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR kupitia taarifa waliyoitoa kwa pamoja jijini Geneva Uswisi na BangKok Thailand, wameeleza wasiwasi mkubwa kufuatia taarifa kwamba boti mbili zilizokuwa zimebeba zaidi ya watu 500 huenda zimezama katika pwani ya Myanmar katika siku za hivi karibuni.
Zaidi ya watoto milioni 23 wengine zaidi ya wale ambao wako tayari kwenye umaskini duniani wanaweza kutumbukia katika umaskini wa kipato ifikapo mwisho wa mwaka huu wa 2025 kutokana na kuendelea kwa mzozo wa Mashariki ya Kati na athari zake kwa biashara ya kimataifa, kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) jijini New York, Marekani.
Sitisho la mapigano kati ya Israeli na Palestina lililotiwa saini Oktoba 10, 2025, limeanza kuleta matumaini mapya kwa wakulima katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu. Baadhi wameanza kurejea mashambani baada ya miezi ya uhamisho na uharibifu mkubwa uliosababishwa na vita.
Uganda leo imeanza rasmi kuhesabu siku 42 kuelekea kutangazwa kumalizika kwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola baada ya mgonjwa wa mwisho aliyethibitishwa kuwa na maambukizi kupimwa mara ya pili na kubainika hana virusi hivyo, kisha kuruhusiwa kutoka hospitalini. Hatua hiyo ni mafanikio muhimu katika juhudi za nchi hiyo kudhibiti mlipuko, imesema taarifa iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO ofisi ya Uganda.