Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kikundi cha watoto wa shule za Kiafrika wakiwa wamevaa sare, baadhi yao wakiwa wamevaa hijabi, wakitunza mimea katika bustani ya shule huko Zanzibar, Tanzania.
© UNICEF

Kijana Ahmad Omar aongoza mabadiliko ya kijani shule ya Kisiwandui Zanzibar

Elimu imepata maana mpya kwa wanafunzi wa shule ya msingi Kisiwandui iliyopo Zanzibar nchini Tanzania, ambapo sasa masomo ya uhifadhi wa mazingira hayajaishia darasani pekee bali yamegeuka kuwa vitendo. Kupitia mradi wa ROTA unaotekelezwa na Shirika la Wakfu wa Elimu juu ya Mengine Yote kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF nchini humo. Rashid Malekela anatupeleka visiwani Zanzibar kufahamu jinsi kijana Ahmad Omar Mohammed anavyoongoza wenzake katika mabadiliko haya.

Sauti
2'35"
Mwanamume na mwanamke wanakimbia kwenye barabara ya lami kupitia eneo la vijijini nchini Kenya, na mashamba ya mahindi kwenye mandhari ya nyuma.
© UNFPA

UNFPA: Ukatili wa Kijinsia kwa wanariadha nchini Kenya waibua wadau, viongozi

Baada ya matukio ya ukatili wa kijinsia, GBV na mauaji ya wanariadha wanawake kutikisa mji wa Iten, nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi, UNFPA linashirikiana na Kituo cha Kukuza Demokrasia na Utawala Bora nchini humo kufanya kazi na makocha, wanariadha, maafisa wa michezo na serikali ya kaunti ili kuimarisha ulinzi kupitia elimu ya utambuzi, uzuiaji na kukabiliana na ukatili wa kijinsia. 

Sauti
2'55"