Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wanawake wawili katika mpangilio wa studio, wakiwa wameketi kwenye meza ya duara wakiwa na maikrofoni, wakishiriki katika majadiliano mbele ya mandhari yenye nembo UN .
UN News/Feissal Kirwa

Wavamizi wote waondoke DRC ili sisi ‘wakongomani’ tuendeleze nchi yetu – Bi. Kibuya

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasiaya Congo, DRC, shirika la kiraia la Congo Notre Avenir, yaani kwa kiswahili, Congo Mustakabali wetu linapigania haki ya amani kwa wanawake ili hatimaye waweze kushiriki katika kuendeleza familia zao kwa kushirikiana na familia zao, wakati huu ambapo mapigano mashariki mwa nchi yamesababisha ukatili ikiwemo ubakaji, na hata wanaume kuacha familia zao na kwenda msituni kupigana.

Rohingya refugees arrive by makeshift raft from Myanmar to Noya Para, Bangladesh.
© UNICEF/Mackenzie Knowles-Coursin

Zaidi ya watu 500 wahofiwa kuzama maji na kufariki dunia pwani ya Myanmar

Mashirika mawili ya Umoja Umoja wa Mataifa lile la Uhamiaji, IOM na la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR kupitia taarifa waliyoitoa kwa pamoja jijini Geneva Uswisi na BangKok Thailand, wameeleza wasiwasi mkubwa kufuatia taarifa kwamba boti mbili zilizokuwa zimebeba zaidi ya watu 500 huenda zimezama katika pwani ya Myanmar katika siku za hivi karibuni.

Mfanyakazi wa UNICEF aliyevalia hijab ya bluu nyepesi na koti, akiwa amevaa glavu za bluu, anapima ukuaji wa mtoto aliyebebwa na mama katika makao ya muda huko Beirut, Lebanoni.
© UNICEF/Fouad Choufany

Mamilioni ya watoto duniani wako hatarini kutumbukia kwenye umaskini

Zaidi ya watoto milioni 23 wengine zaidi ya wale ambao wako tayari kwenye umaskini duniani wanaweza kutumbukia katika umaskini wa kipato ifikapo mwisho wa mwaka huu wa 2025 kutokana na kuendelea kwa mzozo wa Mashariki ya Kati na athari zake kwa biashara ya kimataifa, kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) jijini New York, Marekani.

Wafanyakazi wa afya wakiwa wamevaa vifaa kamili vya kujikinga (PPE) wamesimama ndani ya hema la matibabu wakati wa kukabiliana na mlipuko wa Ebola nchini Uganda.
© WHO/Natalie Ridgard

Uganda yaanza kuhesabu siku 42 kuelekea kutangaza mwisho wa Ebola

Uganda leo imeanza rasmi kuhesabu siku 42 kuelekea kutangazwa kumalizika kwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola baada ya mgonjwa wa mwisho aliyethibitishwa kuwa na maambukizi kupimwa mara ya pili na kubainika hana virusi hivyo, kisha kuruhusiwa kutoka hospitalini. Hatua hiyo ni mafanikio muhimu katika juhudi za nchi hiyo kudhibiti mlipuko, imesema taarifa iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO ofisi ya Uganda.