Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kikundi cha vijana mbalimbali katika Kongamano la Umoja wa Mataifa la Vijana huko Cascais, Ureno, walipunga na kutabasamu kando ya bahari Novemba 25, 2024.
UN News/Eileen Travers

Je, mazungumzo yanaweza kuponya dunia iliyogawika? Muungano unaoongozwa na UN unaweka hoja hiyo mezani

Dunia inavyokaribia mwishoni mwa mwaka 2025, mgawanyiko wa kijiografia unazidi kuongezeka kati ya Kaskazini na Kusini, Mashariki na Magharibi. Ndiyo maana Jukwaa la Riyadh nchini Saudi Arabia linatumika katika Muungano wa Ustaarabu wa Umoja wa Mataifa UNAOC) kama mahali pa kukutanisha serikali, asasi za kiraia, vijana viongozi na wanawake wajenzi wa amani ili kuendeleza juhudi za kuvuka tofauti, kupambana na kutovumilia hotuba za chuki, na kuimarisha kuheshimiana katika dunia yenye nguvu nyingi.

Upatikanaji wa maji ni muhimu ili kuzuia uhamiaji katika maeneo kama vile magharibi mwa Nigeria.
© World Bank/Arne Hoel

Upatikanaji wa maji yanayoweza kurejelezwa kwa mtu mmoja wapungua kwa asilimia 7 katika miaka 10 - FAO

Upatikanaji wa maji safi yanayoweza kurejelezwa kwa mtu mmoja mmoja umepungua kwa kiwango cha asilimia 7 katika muongo mmoja, huku shinikizo likiongezeka katika maeneo yenye uhaba mkubwa wa maji, hii ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya taarifa ya kuonesha picha halisi ya rasilimali maji na matumizi yake duniani,  AQUASTAT 2025 iliyotolewa leo tarehe 12 Desemba 2025 na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, (FAO).