'UM uliopoa' kutunza mazingira Makao Makuu
Kuanzia Ijumaa tarehe mosi Agosti, UM utatekeleza mradi maalumu kwenye majengo ya Makao Makuu yaliopo New York, kwa matarajio ya kuongeza akiba ya fedha za matumizi na kutunza mazingira. Hatua hii inachukuliwa kwa kulingana na juhudi za kimataifa za kukabiliana na matatizo yanayotokana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa, na UM imeamua kuongoza kwenye juhudi hizi kwa vitendo.