Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Nini maana ya Siku Kuu ya Walinzi wa Amani Duniani?

Kila mwaka, tarehe 29 Mei huadhimishwa na UM kuwa ni Siku Kuu ya Kuheshimu Mchango wa Walinzi wa Amani Duniani. Taadhima za mwaka huu zinawakilisha miaka 60 tangu operesheni za ulinzi wa amani za UM kuanzishwa rasmi mnamo tarehe 29 Mei 1948. KM Ban Ki-moon kwenye risala ya kuiheshimu siku hiyo aliwapongeza walinzi wa amani wa kimataifa, waume kwa wake, waliotawanyika katika sehemu mbalimbali za dunia, kwa mchango wao katika kuimarisha utulivu na usalama wa kimataifa.~

Hapa na Pale

KM Ban Ki-moon amesifu na kupongeza azimio liliopotishwa kwenye Mkutano wa kidiplomasiya uliofanyika Dublin, Ireland ambapo wajumbe wa Mataifa 111 waliridhia hati ya mkataba mpya wa kimataifa wa kupiga marufuku matumizi ya vile vibomu vya mtawanyo, na vile vile amehimiza Mataifa Wanachama kuidhinisha haraka mkataba na kuufanya chombo cha sheria ya kimataifa.

Mkariri wa masuala ya ubaguzi ashtumu mashambulio ya wageni Afrika Kusini

Doudou Dienne, Mkariri Maalumu wa UM anayehusika na masuala ya ukabila, ubaguzi wa rangi wa kisasa, chuki za wageni wa nchi na utovu wa ustahamilivu, leo amewasilisha taarifa maalumu yenye kuelezea huzuni alionayo kuhusu kiwango kilichofurutu ada cha yale mashambulio ya chuki yaliofanyika Afrika Kusini karibuni, dhidi ya wahamiaji wa mataifa jirani, na pia dhidi ya kundi la makabila madogo ya wahamiaji yaliopo nchini, hujuma ambazo alisema ziliendelezwa mjini Johannesburg na vile vile kwenye vitongoji jirani, na kusababisha mauaji ya watu zaidi ya 40 na majeruhi kadha.

UM umechukizwa na mauaji katili Darfur ya ofisa wa UNAMID

UM umepokea taarifa zenye kusema ofisa mmoja wa vikosi mseto vya UM na UA katika Darfur, au vikosi vya UNAMID, aliotokea Uganda alikutikana Ijumatano magharibi ameuawa, ndani ya gari ya kazini, ilioegezwa karibu na marikiti ya mji wa El Fasher, Darfur kaskazini, kwa mujibu wa Msemaji wa UNAMID, Noureddine Mezni. Marehemu huyo, Inspekta John Kennedy Okecha tuliarifiwa alipigwa risasi tatu - shingoni, kifuani na kwenye tumbo.

Bei kubwa za chakula zitaendelea kuselelea miaka ijayo,FAO yaonya

Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) kwenye ripoti ya mwaka iliotayarishwa bia na Shirika la la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo (OECD) kubashiria Matarajio ya Kilimo duniani imethibitisha kwamba bei za bidhaa za kilimo kwenye soko la kimataifa zitaendelea kuwa za kigeugeu katika kipindi kijacho.