Nini maana ya Siku Kuu ya Walinzi wa Amani Duniani?
Kila mwaka, tarehe 29 Mei huadhimishwa na UM kuwa ni Siku Kuu ya Kuheshimu Mchango wa Walinzi wa Amani Duniani. Taadhima za mwaka huu zinawakilisha miaka 60 tangu operesheni za ulinzi wa amani za UM kuanzishwa rasmi mnamo tarehe 29 Mei 1948. KM Ban Ki-moon kwenye risala ya kuiheshimu siku hiyo aliwapongeza walinzi wa amani wa kimataifa, waume kwa wake, waliotawanyika katika sehemu mbalimbali za dunia, kwa mchango wao katika kuimarisha utulivu na usalama wa kimataifa.~