Wadau lazima watimize wajibu wao kurejesha amani DRC: Lacroix
Ili amani ya kweli na ya kudumu iweze kurejea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ni lazima wadau wote wa kisiasa ikiwemo serikali, chama tawala, wapinzani, asasi za kiraia na tume ya uchaguzi watimize wajibu wao katika kuhakikisha maandalizi ya uchaguzi mkuu yanaendelea kwa wakati kama ilivyopangwa.