Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MKUTANO WA 73 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA

MKUTANO WA 73 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
MJADALA MKUU WA UNGA73

Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 25 septemba 2018 hadi Oktoba mosi 2018. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Kifua Kikuu, Ulinzi wa Amani, tukio maalum la kumuenzi hayati Nelson Mandela na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs.

Kikao cha Kwanza cha Baraza Kuu la ushirikiano wa mataifa (sasa Umoja wa Mataifa) Hii ni tarehe 10 January mwaka 1946 huko London, Uingereza. Ni katka kikao hiki, Brazil ilikuwa mjumbe wa Baraza Kuu na lile la usalama.
UN /Marcel Bolomey

Kwanini Brazil huwa ya kwanza kuhutubia UNGA?

Kawaida ni rais wa Brazil ndiye hufungua vikao vya ngazi za juu katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Lakini ni kwa nini? Utaratibu huu ulianza katika kikao cha mwanzo kabisa kilichofanyika mjini London, Uingereza Januari 10 mwaka 1946. Tangu wakati huo Brazil imekuwa kila mara inakuwa ya kwanza katika ratiba za viongozi kuhutubia mjadala wa wazi wa Baraza hilo unaofanyika kila mwezi Septemba.
 

United Nations Postal Administration (UNPA)

Mandela kuenziwa leo kwenye UN; Azimio maalum kupitishwa

Leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanapitisha azimio la kumuenzi aliyekuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela.

Hayati Mandela angalikuwa hai mwaka huu, angalikuwa anatimiza umri wa miaka 100 tangu kuzaliwa kwake.

Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imezungumza na Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Modest Mero na kumuuliza kiini hasa cha nchi wanachama kuamua kupitisha azimio hilo kuhusu Mandela ambapo amesema.

Sauti
3'22"
Wanawake wawili ambao wanapata matibabu ya kifua kikuu mjini Addis Ababa , Ethiopia.
The Global Fund/John Rae

Maambukizi ya kifua kikuu yalipungua 2017: WHO

Ripoti mpya ya  shirika la afya ulimwenguni WHO kuhusu hali ya ugonjwa wa  kifua kikuu duniani, TB  inasema kuwa  idadi ya watu waliougua kifua kikuu au kufariki dunia mwaka jana  ilikuwa ni ndogo ingawa bado mataifa mengi hayachukui  hatua za kutosha kuweza kutokomeza ugonjwa huo  ifikapo mwaka wa 2030.