Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 25 septemba 2018 hadi Oktoba mosi 2018. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Kifua Kikuu, Ulinzi wa Amani, tukio maalum la kumuenzi hayati Nelson Mandela na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs.
MKUTANO WA 73 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Tutumie busara za Mandela kukabili changamoto za sasa- Guterres
Umoja wa Mataifa leo umepitisha azimio la kumuenzi Nelson Mandela kutokana na mchango wake katika kusongesha utu, amani na haki za binadamu siyo tu nchini mwake bali duniani kote kwa ujumla. Taarifa zaidi na Grace Kaneiya.
Kwanini Brazil huwa ya kwanza kuhutubia UNGA?
Kawaida ni rais wa Brazil ndiye hufungua vikao vya ngazi za juu katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Lakini ni kwa nini? Utaratibu huu ulianza katika kikao cha mwanzo kabisa kilichofanyika mjini London, Uingereza Januari 10 mwaka 1946. Tangu wakati huo Brazil imekuwa kila mara inakuwa ya kwanza katika ratiba za viongozi kuhutubia mjadala wa wazi wa Baraza hilo unaofanyika kila mwezi Septemba.
Kisasi cha Mandela baada ya kutoka gerezani ni cha kuigwa- Dkt. Salim
Mwanadiplomasia nguli ambaye amewahi kufanya kazi na hayati Mzee Nelson Mandela azungumzia upekee aliokuwa nao mwendazake huyo ambaye leo anaenziwa na UN
Mandela kuenziwa leo kwenye UN; Azimio maalum kupitishwa
Leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanapitisha azimio la kumuenzi aliyekuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela.
Hayati Mandela angalikuwa hai mwaka huu, angalikuwa anatimiza umri wa miaka 100 tangu kuzaliwa kwake.
Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imezungumza na Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Modest Mero na kumuuliza kiini hasa cha nchi wanachama kuamua kupitisha azimio hilo kuhusu Mandela ambapo amesema.
Dunia ijifunze kusamehe kama alivyofanya Mandela- Balozi Mero
Leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanapitisha azimio la kumuenzi aliyekuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela.
Je wajua mapana na marefu ya rungu la kuongozea mikutano ya UNGA?
Rungu la rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA, linalotumiwa kuongozea mikutano lilitolewa kama zawadi ya Iceland kwa Umoja wa Mataifa.
Maambukizi ya kifua kikuu yalipungua 2017: WHO
Ripoti mpya ya shirika la afya ulimwenguni WHO kuhusu hali ya ugonjwa wa kifua kikuu duniani, TB inasema kuwa idadi ya watu waliougua kifua kikuu au kufariki dunia mwaka jana ilikuwa ni ndogo ingawa bado mataifa mengi hayachukui hatua za kutosha kuweza kutokomeza ugonjwa huo ifikapo mwaka wa 2030.
Afrika tutaangazia amani na maendeleo endelevu - Balozi Modest Mero.
Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unafunguliwa rasmi hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.
Lajčák akabidhi kijiti cha kuongoza Baraza Kuu Maria Espinosa
Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umetamatishwa hii leo ambapo aliyekuwa rais wake Miroslav Lajčák ametaja mambo sita muhimu aliyobaini wakati wa uongozi wake tangu mwezi Septemba mwaka jana.
UNGA73 yaanza rasmi, rais wake asema mabadiliko ya tabianchi hayakomi ijumaa
Rais wa mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ulioanza rasmi hii leo Maria Fernanda Espinosa ametaja mambo muhimu yatakayoongoza utendaji wake kwa kipindi kizima cha mwaka mmoja.