Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 25 septemba 2018 hadi Oktoba mosi 2018. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Kifua Kikuu, Ulinzi wa Amani, tukio maalum la kumuenzi hayati Nelson Mandela na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs.
MKUTANO WA 73 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Hebu na tuyaangazie mambo chanya barani Afrika- Kagame
Rais Paul Kagame wa Rwanda amehutubia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kutaka kile alichokiita kuwa maendeleo chanya barani Afrika kisipuuzwe licha ya changamoto zinazokumba bara hilo.
Ushirikiano wa kimataifa ndio suluhu ya changamoto zinazotukabili:Espinosa
Misingi mikuu mitatu ambayo ni uongozi bora, kushirikiana majukumu na kuchukua hatua za pamoja ni muhimu kwa mustakhbali wa dunia amesema Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Maria Espinosa.
Si hiyari, ni lazima kulikabili jinamizi la mabadiliko ya tabia nchi:Guterres
Mjadala wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kikao cha 73 umefunguliwa rasmi hii leo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres. Wawakilishi kutoka nchi 193 wanachama, mashirika ya kimataifa, asasi za kiraia na wadau wengine wa maendeleo wakikutana kwa lengo la kuhakikisha ajenda ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa inatimia ifikapo 2030.
Kwa faida ya Afrika mwelekeo wa uhamiaji lazima ubadilike:UNCTAD
Madiliko kuhusu suala la uhamiaji barani Afrika ni lazima, kwani yatasaidia kwanza kubadili fikra na mtazamo kuhusu suala la uhamiaji, lakini pia kusongesha mbele gurudumu la maedeleo endelevu au SDG’s kwa mataifa ya bara hilo.
Kando ya UNGA, ulinzi wa amani nao kuangaziwa kwa kina
Mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukianza leo, wakuu wa nchi na viongozi wa serikali wa nchi zinazochangia kwenye operesheni za ulinzi wa amani wanakutana kujadili jinsi ya kukabiliana na changamoto za ulinzi wa amani.
Madiba hakupenda makuu
Ikiwa leo Umoja wa Mataifa unafanya tukio maalum kuhusu miaka 100 tangu kuzaliwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, hayati Nelson Mandela, mwanadiplomasia nguli nchini Tanzania na ambaye amewahi kuhudumu barani Afrika na Umoja wa Mataifa amemmwagia sifa hayati Mandela akisema kuwa alikuwa kiongozi shupavu ambaye kisasi chake baada ya kufungwa kilikuwa ni kuona watu wake wanaendelea.
Viongozi wa sasa waige mfano wa Mandela- Dkt. Salim
Mwendazake Mzee Nelson Mandela, angalikuwa anatimiza umri wa miaka 100 mwaka huu iwapo angalikuwa hai. Ingawa hayupo, bado kile alichokifanya wakati wa uhai wake kinakumbukwa na kuenziwa siyo tu nchini mwake na barani Afrika bali pia katika Umoja wa Mataifa ambako ajenda alizokuwa anatetea ni mambo ambayo ni msingi wa Umoja wa Mataifa.
Matarajio yetu kwa dunia iliyo sawa ni kwenu vijana: Guterres
Umoja wa Mataifa leo umezindua mkakati wake mpya wa kuimarisha mchango wa takribani vijana bilioni 2 duniani kwa lengo kukuza amani, uadilifu pamoja na kuwa na dunia endelevu.
Kuanza kwa UNGA ni matokeo ya maandalizi ya takribani mwaka mmoja
Mkutano wa kila mwaka wenye lengo la kuimarisha diplomasia ya kimataifa hufanyika kwa juma moja wakati wa kuanza mwa mkutano wa Baraza kuu la Umoja wa mataifa lakini maandalizi huchukua miezi kadhaa. Hakuna ambalo halizingatiwi katika tukio ambalo linavuta hisia za mamilioni ya watu duniani kote.
Uhamiaji Afrika si karaha bali ni faida:UNCTAD
Kuuchukulia uhamiaji kama ni tatizo si fikra nzuri , kwani unahamiaji una faida nyingi, kwa wahamiaji wenyewe lakini pia kwa jamii zinazowahifadhi, iwe katika masuala ya kiuchumi, utamaduni na hata maendeleo kwa mujibu wa Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD