Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 25 septemba 2018 hadi Oktoba mosi 2018. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Kifua Kikuu, Ulinzi wa Amani, tukio maalum la kumuenzi hayati Nelson Mandela na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs.
MKUTANO WA 73 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Kwa ujumla usalama umerejea Burundi na wakimbizi wanarudi: Nibigira
Waziri wa mambo ya nje wa Burundi amesema kwa ujumla hali ya usalama na utulivu imerejea Burundi na kilichosalia ni matukio madogomadogo ya utovu wa nidhamu.
Vita vyetu dhidi ya ugaidi vinakaribia ukingoni: Syria
Naibu waziri mkuu na waziri wa mambo ya nje wa Syria Walid al-Muallem amesema vita vya nchi yake dhidi ya ugaidi vinaelekea ukingoni akishukuru ujasiri, dhamira, umoja wa watu wa Syria, jeshi la nchi hiyo, msaada wa marafiki na washirika wao.
Mshikamano ndio suluhu pekee ya maendeleo duniani:Chad
Ili kuhakikisha kunakuwa na maendeleo kwa wote duniani , hakuna chaguo lolote la kufikia azma hiyo isipokuwa kufanya kazi pamoja , kuibua vitosho vilivyopo na kukabiliana na changamoto zinazoughubika ulimwengu kwa kuzingatia misingi ya kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa.
Darfur ya sasa ni bora kuliko miaka 10 nyuma, lakini kazi bado ipo – Naibu Katibu Mkuu UN
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bi. Amina Mohammed amesema hivi sasa jimbo la Darfur ya sasa nchini Sudan inaonekaana ni tofauti na Darfur ya miaka 10 iliyopita wakati ambapo Muungano wa Afrika, AU wa Afrika na Umoja wa Mataifa kwa pamoja walituma vikosi vya kulinda amani.
Sudan Kusini tunapiga hatua,asanteni sana- Gai
Mwaka jana nilisimama mbele yenu nikiwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa nchi iliyogubikwa na vita. Leo hii nimesimama tena mbele yenu kama shuhuda wa kile ambacho wanachama wa chombo hiki adhimu wamesaidia kufanikisha ndani ya Jamhuri ya Sudan Kusini.
Ni kauli ya Taban Deng Gai, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan Kusini aliyotoa wakati akihutubia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaoendelea kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani.
Sudan Kusini ya mwaka jana si ya mwaka huu, shukrani UN, AU na wadau- Gai
Mwaka jana nilisimama mbele yenu nikiwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa nchi iliyogubikwa na vita. Leo hii nimesimama tena mbele yenu kama shuhuda wa kile ambacho wanachama wa chombo hiki adhimu wamesaidia kufanikisha ndani ya Jamhuri ya Sudan Kusini.
Uhamiaji sio shida Afrika la msingi kutovunja sheria- Rais Nyusi
Suala la uhamiaji likiendelea kuibua vuta nikuvute, Msumbiji imesema kuwa la msingi ni watu kufuata sheria kwani uhamiaji umekuwepo na utaendelea kuwepo.
Uganda itaendelea kuwa kimbilio la wakimbizi- Rugunda
Sisi ni kizazi cha kutokomeza njaaTunaweza kuwa kizazi cha kwanza kufanikiwa kutokomeza njaa, kama ambavyo tunaweza kuwa kizazi cha mwisho kuikoa dunia.
Tunaunga mkono ushirikiano wa kimataifa- Tanzania
Tanzania imetaka hatua za dhati zichukuliwe ili kuokoa hoja ya ushirikiano wa kimataifa ambao hivi sasa uko mashakani.
Hongera Sudan Kusini kwa kuchukua hatua zaidi kuwalinda watoto:Gamba
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya watoto na migogoro ya Silaha, Bi. Virginia Gamba, ameipongeza serikali ya Sudan Kusini kwa kuongeza kipengele cha hiyari kwenye mkataba kuhusu haki za mtoto katika ushirikishaji kwenye migogoto ya kivita (OPAC).