Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Rais wa Sudan asema deni la nje linairudisha nyuma nchi yake kufikia maendeleo
Deni la nje ni kikwazo kikubwa kinachozuia ukuaji wa kiuchumi na kijamii nchini Sudan na pia linazuia kutimiza malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa SDGs amesema leo Rais wa serikali ya mpito wa Sudan Abdel-Fattah AlBurhan Abdelrahman Al-Burhan wakati akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu kikao cha 77 jijini New York Marekani.
Amani inaimarika Sudan Kusini lakini bado tuna changamoto: Agany
Amani nchini Sudan Kusini inaendelea kuimarika huku idadi kubwa ya wakimbizi wa ndani wameanza kurejea katika makazi yao kwenye maeneo ambako utulivu umerejea na serikali inafanya kila iwezalo kuhakikisha mkataba wa amani unadumiswa amesema makamu wa Rais wa Sudan Kusini Hussein Abdelbagi Akol Agany akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza kuu hii leo mjini New York Marekani.
Vita ya Ukraine imetuletea adha dunia nzima: Azali Assoumani
Rais wa kisiwa cha Comoro Azali Assoumani akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu kikao cha 77 amesema jumuiya ya kimataifa hivi sasa inakabiliwa na changamoto lukuki, kuanzia athari za kiafya kama janga la COVID-19 ambalo linaingia mwaka wa tatu ssasa, mabadiliko ya tabianchi hadi vita ya Ukraine ambayo imeleta adha kwa dunia nzima.
Msifurishe dunia hii leo, wala msiizamishe kesho- Ujumbe wa Katibu Mkuu wa viongozi wa dunia
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani hii leo ikiwa ni kuelekea Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la UN unaoanza wiki ijayo akisema ujumbe wake mkuu kwa viongozi watakaoshiriki ni dhahiri ya kwamba wachukue hatua kupunguza kiwango cha joto duniani.
Ukame na mabadiliko ya tabianchi vyazidisha adha ya maji Afrika:WMO
Inaonyesha jinsi hali mbaya ya hewa na mabadiliko ya tabianchi yanavyodhoofisha afya na usalama wa binadamu, uhakika wa chakula na maji na maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
07 SEPTEMBA 2022
Katika jarida la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Katibu Mkuu UN atoa wito kwa ushirikiano wa kimataifa kukabiliana na uchafuzi wa hali ya hewa katika siku ya kimataifa ya hewa safi kwa ajili ya anga ya bluu
-Hatuwezi kusubiri hadi baa la njaa litangazwe Somalia tunafanya kila tuwezalo kuwanusuru Wasomali limesema shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP
Hewa inayopaswa kutupa uhai sasa inatupatia maradhi waonya wataalam wa UN
Siku ya kimataifa ya hewa safi kwa anga ya bluu, inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 7 Septemba, mwaka huu inafanyika katika ulimwengu ambao karibu hewa yote tunayopumua imechafuliwa, na takriban watu milioni saba hufa kutokana na uchafuzi wa hewa kila mwaka kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
UNICEF yawasilisha sehena ya misaada kwa ajili ya watoto na wanawake walioathirika na mafuriko nchini Pakistan
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani UNICEF hii leo limewasilisha tani 32 za dawa za kuokoa maisha na vifaa vingine vya dharura ili kusaidia watoto na wanawake walioathiriwa na mafuriko kote nchini Pakistan.
Watu 34,000 waathirika na mafuriko Chad:UN
Watu 34,000 wameathirika na mafuriko katika majimbo 11 kati ya 23 nchini Chad kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na mashirika ya Umoja wa Mataifa.