Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Baada ya vuta ni kuvute ya wiki mbili muafaka wafikiwa COP24
Baada ya wiki mbili za majadiliano ya makundi zaidi ya 200 yaliyokusanyika Katowice, Poland kwa ajili mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi , COP24 ,yameidhinisha muongozo wa utekelezaji wa mkataba wa Paris wa mwaka 2015, wenye lengo la kupunguza ongezeko ka joto duniani kuwa nchini ya nyuzi joto 2 ikilinganishwa na viwango vya kabla ya wakati wa viwanda.
Kuna matumaini kwenye majadiliano ya mabadiliko ya tabianchi-COP24
Majadiliano ya mbinu za kupambana na mabadiliko ya tabianchi yanaendelea mjini Katowice nchini Poland huku washiriki wakionyesha matumaini ya azma ya mkutano huo wa 24 wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabia nchi au COP24.
Mama Katarina ni mfano wa jinsi nishati endelevu inavyobadili maisha-FAO
Nchini Tanzania mradi mpya wa shirika la chakula na kilimo duniani, FAO wa kuzalisha umeme kwa kutumia samadi ya wanyama, umekuwa mkombozi kwa wafugaji wa ng’ombe ambao kwa muda mrefu wamejikuta kiwango kikubwa cha maziwa kinaharibika kutokana na ukosefu wa majokofu ya kuhifadhi.
UN na sekta ya michezo kudhibiti mabadiliko ya tabia nchi:COP24
Sekta ya michezo na kitengo cha Umoja wa Mataifa cha kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi leo wamezindua mfumo wa kuyakusanya mashirika ya michezo, timu, wanamichezo na mashabiki kwatika juhudi za pamoja za kuchagiza na kuchukua hatua ili kufikia malengo ya mkataba wa Paris .
Mradi wa Benki ya Dunia Niger wakomesha hamahama ya wananchi kutokana na ukame
Wakati mabadiliko ya tabianchi yakiendelea kuwa tishio kwa watu maskini zaidi duniani Benki ya dunia imetangaza kuwekeza dola bilioni 200 katika kipindi cha miaka mitano ijayo kwa ajili ya kuweka mazingira bora na kujengea stahamala nchi zilizoathirika. Mojawapo ya nchi ambako Benki ya Dunia imewekeza ni Niger.
Mamia wakielekea Marrakech, CO24 nayo yajadili tabianchi na uhamiaji
Wakati mamia ya watunga sera wakikusanyika huko Marrakech nchini Morocco kwa ajili ya kukubaliana juu ya mkataba mpya wa kimataifa kuhusu uhamiaji, mkutano wa 24 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP24 huko Katowice Poland, nao unajikita katika njia thabiti za kusaidia nchi kukabiliana na ukimbizi wa ndani utokanao na madhara ya mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ukosefu wa maji, mafuriko, vimbunga na kuongezeka kwa kina cha maji ya bahari
Akiwa COP24 Guterres ataja mambo manne muhimu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumza katika ufunguzi wa mkutano wa 24 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP24 huko Katowice, Poland hii leo na kutaja mambo makuu manne anayoamini ni muhimu ili kubadili mwelekeo wa sasa wa tabianchi.
03 Disemba 2018
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa leo Siraj Kalyango anaangazia
-Kuanza kwa mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya tabia nchi COP 24, Umoja wa Mataifa ukihizima ufadhili na kasi ya kupambana na mabadiliko hayo
-Siku ya Kimataifa ya watu wenye ulemavu , je ni yapi yanayomkabili mtu anayeishi na ulemavu? tutabisha hodi Kagera Tanzania
-Ngozi ya samaki aina ya sangara mali kubwa nchini Kenya kulikoni
-Makala tunaendelea na ibara za tamko la haki za binadamu leo ni ibara ya 23 ikiangazia haki za wafanyakazi wa ndani
Teknolojia ya nyuklia yaleta mbegu mpya za mpunga na maharage
Aina mpya ya mbegu za mpunga na maharagwe ambazo zinastahimili mabadiliko ya tabianchi zimeanza kusambazwa ili kusaidia wakulima kupanda mazao hayo ambayo ni chakula tegemezi kwenye maeneo hayo.
Viashiria vya mabadiliko ya tabianchi na madhara yake vyaendelea 2018
Hali ya joto duniani imeendelea kuongezeka mwaka 2018 huku wastani wa kiwango cha joto duniani kote ikitarajiwa kushika nafasi ya nne na kuvunja rekodi.