Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Kikao chamwisho cha mkutano wa COP24 Katowice, Poland,16 Disemba 2018.
UNFCCC/James Dowson

Baada ya vuta ni kuvute ya wiki mbili muafaka wafikiwa COP24

Baada ya wiki mbili za majadiliano ya makundi zaidi ya 200 yaliyokusanyika Katowice, Poland kwa ajili mkutano wa Umoja wa  Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi , COP24 ,yameidhinisha  muongozo wa utekelezaji wa mkataba wa Paris wa mwaka 2015, wenye lengo la kupunguza ongezeko ka joto duniani kuwa nchini ya nyuzi joto 2 ikilinganishwa na viwango vya kabla ya wakati wa viwanda.

Kimbunga Hagupit kilipopiga Ufilipino tarehe 5-6 Desemba 2014, hali ilikuwa mbaya kwani nchi  hiyo bado ilikuwa haijasahau madhara ya kimbunga Haiyan kilichotokea Novemba 2013.
OCHA/Jennifer Bose

Mamia wakielekea Marrakech, CO24 nayo yajadili tabianchi na uhamiaji

Wakati mamia ya watunga sera wakikusanyika huko Marrakech nchini Morocco kwa ajili ya kukubaliana juu ya mkataba mpya wa kimataifa kuhusu uhamiaji, mkutano wa 24 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP24 huko Katowice Poland, nao unajikita katika njia thabiti za kusaidia nchi kukabiliana na ukimbizi wa ndani  utokanao na madhara ya mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ukosefu wa maji, mafuriko, vimbunga na kuongezeka kwa kina cha maji ya bahari

 

03 Disemba 2018

Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa leo Siraj Kalyango anaangazia

-Kuanza kwa mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya tabia nchi COP 24, Umoja wa Mataifa ukihizima ufadhili na kasi ya kupambana na mabadiliko hayo

-Siku ya Kimataifa ya watu wenye ulemavu , je ni yapi yanayomkabili mtu anayeishi na ulemavu? tutabisha hodi Kagera Tanzania

-Ngozi ya samaki aina ya sangara mali kubwa nchini Kenya kulikoni

-Makala tunaendelea na ibara za tamko la haki za binadamu leo ni ibara ya 23 ikiangazia haki za wafanyakazi wa ndani

Audio Duration
14'42"