Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Katibu Mkuu António Guterres akizungumza kwenye kongamano la dunia la muungano  wa R20 nchini Austria
UNIS Vienna/Nikoleta Haffar

Komesheni ruzuku kwa sekta ya mafuta na matumizi ya fedha za watoa ushuru kutokomeza dunia- Guterres

Tunahitaji kutoza kodi uchafuzi wa hewa lakini sio watu na kukomesha ruzuku kwa sekta ya mafuta,  amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres hii leo Jumanne kwenye kongamano la dunia la muungano  wa R20, shirika  linaloungwa mkono na Umoja wa Mataifa lilioanzishwa na aliyekuwa gavana wa California nchini Marekani Arnold Schwarzenegger.

©FAO/Christabel Clark

Hatua dhidi ya athari ya mabadiliko ya tabianchi Kenya

Dunia imeadhimisha siku ya familia Mei 15, mwaka huu ikibeba kaulimbiu familia na hatua katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Hatua hii ni kufuatia mabadiliko ya tabiachi yanayoshuhudiwa duniani kote huku athari zake zikiwakumba watu wote.  Grace Kaneiya amezungumza na familia moja huko nchini Kenya ambao wanashiriki kilimo lakini pia ni wafugaji huku wakichukua hatua kulinda mazingira, Je wamechukua hatua zipi? Basi sikiliza makal ifuatayo kwa undani zaidi. 

Sauti
5'26"