Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Dkt Agnes Kijazi: Hali ya hewa haina mipaka, ni muhimu nchi zote tushirikiane.
Mkutano wa sayansi, teknolojia na ubunifu unakunja jamvi hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ambapo wabunifu wa sayansi na wabobevu wa teknolojia wamejadiliana kwa siku mbili. Miongoni mwao ni Dkt Agnes Kijazi, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya hali ya hewa nchini Tanzania ambaye ni mmoja wa wajumbe 10 wa jopo la ngazi ya juu la Umoja wa Mataifa la kutoa ushauri kuhusu jinsi sayansi na teknolojia inavyoweza kutumika kusongesha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.
Guterres aendelea kupigia chepuo hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliyeko ziarani huko nchi za visiwa vya Pasifiki, leo amehutubia mkutano wa jukwaa la viongozi wa visiwa vya ukanda huo akiangazia mambo makuu mawili ambayo ni changamoto siyo tu kwa eneo hilo bali ulimwengu mzima kwa ujumla.
Kuna mambo manne ya kuzingatia katika vita vya mabadiliko ya tabianchi:Guterres
Vijana nchini New Zealand wamepongezwa na Umoja wa Mataifa kwa kazi nzuri na mchango wao mkubwa katika vita dhidi ya mabadiliko ya tabianchi , huku wakiaswa kuongeza juhudi na kuwa wabunifu Zaidi kwa kusaka suluhu mbadala kwa ajili ya changamoto hii inayoighubika duniani.
Heko vijana wa New Zealand, dunia tuzingatie mambo manne katika mabadiliko ya tabianchi- Guterres
Vijana nchini New Zealand wamepongezwa na Umoja wa Mataifa kwa kazi nzuri na mchango wao mkubwa katika vita dhidi ya mabadiliko ya tabianchi , huku wakiaswa kuongeza juhudi na kuwa wabunifu Zaidi kwa kusaka suluhu mbadala kwa ajili ya changamoto hii inayoighubika duniani.
Heko New zealand kwa vita dhidi ya silaha, chuki, na mabadiliko ya tabianchi:UN
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterees yupo ziarani , Auckland, mjii mkuu wa New Zealand hii leo, ambapo kwenye mkutano wa pamoja na Waziri Mkuu wa New Zealand, Jacinda Arden mbele ya waandishi wa habari amesisitiza ushirikiano wake na waathirika wa mashambulizi dhidi ya msikiti katika mji wa Christchurch mwezi Machi yaliyokatili maisha ya watu 51 na kujeruhi wengi wengine.
Chonde chonde wanachama hizi ndio hatua tunazopaswa kuchukua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:UN
Kabla ya mkutano wa kimataifa wa mabadilkiko ya tabianchi ulioitishwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Giuterres mwezi Septemba mwaka huu, leo Umoja wa Mataifa na mashirika yake wameafikiana hatua madhubuti za kuchukua.
Kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, usalama na amani ni muhimu katika kufikia maendeleo Afrika-AU, UN
Mabadiliko ya tabianchi ni moja ya masuala ambayo yataathiri ukuaji wa uchumi wa bara Afrika iwapo uchafuzi wa mazingira hautapunguzwa kwa asilimia 45 kufikia mwaka 2030 na kutokomezwa kabisa ifikapo mwaka 2050 amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akihutubia waandishi wa habari Jumatatu alasiri jijini New York, Marekani.
Teknolojia ya asili ya wafugaji inasaidia mnepo wa mabadiliko ya tabianchi:TANIPE
Changamoto za mabadiliko ya tabianchi kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa hazichagui wala hazibagui taifa au jamii utokayo zinamuathiri kila mtu duniani na ndio maana wito unatolewa kila uchao kuchukua hatua zote stahiki kujenga mnepo dhidi ya zahma hiyo kote duniani. Wito huo hivi sasa unaitikiwa sio tu na serikali mbalimbali kuweka será na mikakati , bali pia wadau wote wakiwemo asasi za kiraia ,sekta binafsi, jamii na hata mashirika ya kijamii.
Wanawake Uganda, vinara wa kuwalinda Sokwe wasitoweke.
Kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo mabadiliko ya tabianchi yaliyosababisha binadamu kusogea zaidi katika makazi asili ya wanyama, mara kadhaa binadamu na wanyama wameingia katika mgogoro ambao unaziathiri pande zote mbili. Migogoro hiyo ni pamoja na wanyama kuvamia makazi ya binadamu na hata kuharibu mashamba huku binadamu nao wakisambaratisha makazi ya wanyama.
Bado inawezekana kudhibiti mabadiliko ya tabianchi na kuilinda dunia:UN
Ulinzi wa sayari dunia unahitajika haraka hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.