Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Ushiriki wa baba mtoto anapozaliwa una faida zake

Ni kawaida barani Afrika kushuhudia mama anapotaka kujifungua kuwa hospitali peke yake, tofauti na mataifa mengi yaliyoendelea ambapo baba ana nafasi yake katika kushuhudia mwanae akizaliwa. Nchini Uganda mambo yameanza kubadilika na wanaume wametambua umuhimu wa kuwa sanjari na kina mama au wake zao wanapojifungua. Kwa undani zaidi ungana na mwandishi wetu John Kibego katika makala hii ya wanawake na uzazi nchini humo.

Bei za vyakula masokoni zimezidi kupanda kila uchao-Burundi

Wakati Ulimwengu ukichagiza uwekezaji zaidi kwenye chakula na  maendeleo ya vijijini  ili kukabiliana na njaa, hata hivyo katika baadhi ya maeneo watu  wameendelea kulalamikia uhaba  mkubwa wa chakula.

Nchini Burundi , siku ya chakula duniani imeadhimihswa  wakati bei za  vyakula masokoni zimezidi kupanda kila uchao.

Mwandishi wetu wa maziwa makuu  Ramadhani KIBUGA makuu ametembelea soko moja la mjini Bujumbura na kutuandalia taaarifa hii.

Jamii yachukua jukumu kulinda vyanzo vya maji Tanga, Tanzania

Athari za mabadiliko ya tabianchi ni dhahiri katika jamii kufuatia matukio mbali mbali yanayoshuhudiwa.

Ni kwa mantiki hiyo ambapo baadhi ya jamii ya watu wa muheza mkoa wa Tanga nchini Tanzania wameamua kutunza mazingira kwa sababu hali ya kilimo, ufugaji na maji si nzuri kwao, na katika kulifahamu hilo wameunda umoja wao ujulikanao kwa jina la UWAMAKIZI yaani Umoja wa Wakulima wa Hifadhi Mazingira Kihugwi Zigi wakiwa na lengo la kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Kampeni ya kutokomeza Malaria ishirikishe wananchi- Dkt. Winnie

Nchi 8 zilizo kusini mwa jangwa la Sahara, zimechukua hatua za kipekee ili kuondokana na ugonjwa wa Malaria ifikapo mwaka 2030. Nchi hizo kupitia wakuu wa  nchi zao wameazimia kwa kufanya yale ambayo yanaonekana ni magumu. Mathalani kutenga bajeti ili kukidhi mahitaji ya kukabiliana na Malaria. Halikadhalika, kwa kuzingatia kuwa ni nchi jirani, basi wana ushirikiano kuhakikisha kuwa kutokomeza malaria nchi moja haiwi chanzo cha kuhamishia ugonjwa huo nchi nyingine. Nchi hizo ni Botswana, Msumbiji, Namibia, Afrika Kusini, Swaziland, Zambia na Zimbabwe wakipatia ubia awo #Elimination8.

(Picha: Idhaa ya Kiswahili/Grace Kaneiya)

Usipokuwa tayari kubadilika hakuna awezaye kukubadilisha- Rocky Dawuni

Malengo ya maendeleo endelevu yaani SDGs yapo 17 na Umoja wa Mataifa unatumia kila mbinu kuhakikisha kuwa kila mkazi wa dunia hii anayafahamu na anashiriki kuyatekeleza pale alipo. Viongozi wanapiga mbiu lakini mwitikio kutoka kwa wananchi unahitaji utayari wao. Hii ina maana kwamba wananchi waelewe umuhimu wa SDGs kwenye maisha yao na ndipo wasimame kidete  kuyatekeleza. Ni katika muktadha huo Umoja wa Mataifa kupitia mfuko wake, UN Foundation unatumia wanamuziki kama vile Rocky Dawuni, mwanamuziki kutoka Ghana na pia balozi mwema wa mfuko huo, kuchagiza malengo hayo.

Vijana wanaokabiliana na tatizo la ajira kujihusisha na miradi ya uvuvi Burundi

Huko Burundi,  Kundi la vijana  limeanzisha maradi wa kujikomboa kutoka  katika hali ya umasikini  kwa kuanzisha  kazi ya uvuvi  bwawani.

Vijana hao saba wa mkoani Bubanza kaskazini magharibi mwa Burundi walianza na mabwawa madogo madogo ya uvuvi , lakini kwa sasa wamefikia  viwango vikubwa vya uzalishaji wa samaki8. Pesa inayotokana  na mradi  huo imekuwa  inasaidia kuwasomesha  vijana  hao katika  vyuo vikuuu.

Jumuiya ya Madola kusongesha maendeleo ya wanawake: Dkt. Ojiambo

Kituo cha biashara cha kimataifa kilicho chini ya kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa, UNCTAD kiliandaa mikutano kadhaa kando mwa mjadala wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, #UNGA72 uliofikia tamati siku ya Jumatatu. Katika moja ya vikao hivyo, washiriki walipata maelezo ya mafanikio ya mpango wa UNCTAD wa #SheTrades ambao unatoa jukwaa kwa wanawake wajasiriamali kubadilishana taarifa na bidhaa wanazouza kupitia intaneti. Miongoni mwa walioshiriki vikao hivyo ni Dkt.

Tukihifadhi mazingira leo tunaepuka gharama kubwa Kesho

Wana mradi wa kuruwitu kutoka Kilifi Mombasa nchini Kenya, wametoa wito wa kuhifadhi mazingira leo ili kuepuka athari zake katika kizazi kijacho. Shida Magunda na Katana Ngala Hinzano wako katika mradi wa kuhifadhi mazingira ya bahari Mombasa kwa kutumia uzalishaji wa samaki. Mradi wao ambao ni wa kwanza nchini Kenya pi umetunukiwa tuzo ya mazingira ya Equator inayotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP na Equator initiative. Wamezungumza na Flora Nducha na Katana Ngala anaanza kueleza historia ya mradi