Siku ya Kiswahili Duniani ni zawadi ya Tanzania kwenda duniani: Balozi Gastorn
Kutangazwa kuwa na siku maalum ya kuadhimisha lugha ya Kiswahili duniani ni zawadi kubwa kutoka Tanzania kwenda duniani na hii ni furaha kubwa sana amesema mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Profesa Kennedy Gastorn akielezea hisia zake baada ya wiki iliyopita shirika la elimu sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO kupitisha azimio la kuifanya tarehe 7 Julai kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.
(CLIP BALOZI KENENDY)