Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Kenya yaliandikia baraza la usalama ikitaka kesi dhidi ya wakenya sita huko ICC zihairishwe kwa mwaka mmoja

Akizungumza na mkuu wa Idhaa ya Radio ya Umoja wa Mataifa Flora Nducha, balozi wa Kenya kwenye Umoja wa Mataifa Macharia Kamau amesema wanachotaka sio kwamba kesi zifutwe zinazowakabilia maafisa sita wa zamani wa serikali ambao ni Uhuru Kenyatta naibu waziri mkuu, Henry Kosgei, Mohammed Hussein Ali aliyekuwa mkuu wa polisi, William Ruto, Francis Muthaura, na mwandishi habari Joshua Arap sang  bali ziahirishwe kwa mwaka mmoja hadi baada ya uchaguzi mkuu wa mwakani.

Amesema zikiendelea sasa zinaweza kuleta chuki na mgawanyiko mkubwa wakati kampeni za uchaguzi mkuu ujao zi

Itakuwa ni matatizo makubwa serikali ya mpito Somalia ikiongeza muda:Mahiga

Mahiga amesema taifa hilo ambalo linaghbikwa na vita kwa miongo miwili sasa linahitaji kuzingatia mkataba wa amani wa Djibouti, kukamilisha kipindi cha mpito na kuchagua serikali mpya hapo mwezi Agosti mwaka huu.

Amesema nia ya serikali ya mpito inayoongozwa na Rais Sheikh Sharif ambayo inataka kupunguza muda wa bunge na kujiongezea mwaka mmoja kwa sasa iko kwenye tafrani na bunge na haina uwezo wa kuzidisha muda pasi idhibni ya Bunge.

Audio Duration
5'19"

Mahojiano kuhusu hali ya ukame na mapigano Somalia

Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa aliyezuru nchi hiyo hivi karibuni Samshul Bari amesema hali ya ukame na machafuko ya vita baiana ya vikosi vya serikali ya mpito na kundi la wanamgambo wa Al-Shabaab ynawaweka wakimbizi wa ndani na raia wa nchi hiyo katika njia panda.

Kuna tatizo kubwa la maji ya kunywa, upungufu wa chakula na pia madawa kutokana na athari za ukame zilizokwisha katili maisha ya watu, mifugo na kukausha baadhi ya vyanzo vya maji. Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Balozi Augustine Mahiga amezungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii kuhusu hali halisi.

Audio Duration
5'19"

DR Congo, Uganda na MONUSCO wako katika mpango wa kuwafurusha waasi wa Uganda wa ADF/NALU

Opreresheni hii ni ya awamu ya nne baada ya zile zilizoanza katikati ya mwaka jana katika mistu iliyoko chini yam lima Ruwenzori upande wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo jimbo la Kivu ya Kaskazini.

Mwandihi habari mjini Beni Mseke Dide amezungumza na Meja Celestine Ngeleka afisa wa usimamizi na mawasiliano wa operesheni hiyo kutoka jeshi la serikali ya Congo ili kupata ufafanuzi wa operesheni hiyo Mashariki mwa Congo.

(MAHOJIANO NA MEJA CELESTINE)

Mkakati kabambe umewekwa na serikali ya mpito kuinusuru Somalia:Mahiga

Akiwa nchini humo amekutana na Rais Sheikh Sharifu Ahmed na waziri mkuu wa nchi hiyo. wamejadili masuala mbalimbali ikiwemo usalama, tatizo la ukame, misaada na ulinzi, lakini kikubwa zaidi ni mkakati mpya uliowekwa na serikali ya Somalia kumaliza uasi nchini humo na kuleta amani ya kudumua baada ya zaidi ya miongo miwili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Je ni mkakati gani huo tegea sikio mahojiano haya kati ya mkuu wa Idhaa ya redio ya Umoja wa Mataifa Flora Nducha na Balozi Mahiga anayeanza kwa kufafania kwa nini kaenda Somalia ghafla.

Sauti
5'19"