Kenya yaliandikia baraza la usalama ikitaka kesi dhidi ya wakenya sita huko ICC zihairishwe kwa mwaka mmoja
Amesema zikiendelea sasa zinaweza kuleta chuki na mgawanyiko mkubwa wakati kampeni za uchaguzi mkuu ujao zi
Amesema zikiendelea sasa zinaweza kuleta chuki na mgawanyiko mkubwa wakati kampeni za uchaguzi mkuu ujao zi
Ripoti hiyo iitwayo "uniting for universal access" inasisitiza uvumilivu sufuri dhidi ya maambukizi ya HIV, ubaguzi na vifo vitokanavyo na ugonjwa huo.
Rebecca Awiti ni muathirika wa Ukimwi nchini Kenya na pia ni mwanaharakati. Amezungumza na Irene Mwakesi wa Ofisi ya UM Nairobi na kueleza alivyokabili suala hilo:
Mahiga amesema taifa hilo ambalo linaghbikwa na vita kwa miongo miwili sasa linahitaji kuzingatia mkataba wa amani wa Djibouti, kukamilisha kipindi cha mpito na kuchagua serikali mpya hapo mwezi Agosti mwaka huu.
Amesema nia ya serikali ya mpito inayoongozwa na Rais Sheikh Sharif ambayo inataka kupunguza muda wa bunge na kujiongezea mwaka mmoja kwa sasa iko kwenye tafrani na bunge na haina uwezo wa kuzidisha muda pasi idhibni ya Bunge.
Jamii ya Toposa huvuka na kuingia nchini Kenya ikitafuta malisho huku ile ya Turkana ikivuka na kuingia Sudan kutafuta maji. Japhet Kasimbu ni msemaji wa IOM.
(SAUTI YA JAPHET KASIMBU)
Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa aliyezuru nchi hiyo hivi karibuni Samshul Bari amesema hali ya ukame na machafuko ya vita baiana ya vikosi vya serikali ya mpito na kundi la wanamgambo wa Al-Shabaab ynawaweka wakimbizi wa ndani na raia wa nchi hiyo katika njia panda.
Kuna tatizo kubwa la maji ya kunywa, upungufu wa chakula na pia madawa kutokana na athari za ukame zilizokwisha katili maisha ya watu, mifugo na kukausha baadhi ya vyanzo vya maji. Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Balozi Augustine Mahiga amezungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii kuhusu hali halisi.
Opreresheni hii ni ya awamu ya nne baada ya zile zilizoanza katikati ya mwaka jana katika mistu iliyoko chini yam lima Ruwenzori upande wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo jimbo la Kivu ya Kaskazini.
Mwandihi habari mjini Beni Mseke Dide amezungumza na Meja Celestine Ngeleka afisa wa usimamizi na mawasiliano wa operesheni hiyo kutoka jeshi la serikali ya Congo ili kupata ufafanuzi wa operesheni hiyo Mashariki mwa Congo.
(MAHOJIANO NA MEJA CELESTINE)
Akiwa nchini humo amekutana na Rais Sheikh Sharifu Ahmed na waziri mkuu wa nchi hiyo. wamejadili masuala mbalimbali ikiwemo usalama, tatizo la ukame, misaada na ulinzi, lakini kikubwa zaidi ni mkakati mpya uliowekwa na serikali ya Somalia kumaliza uasi nchini humo na kuleta amani ya kudumua baada ya zaidi ya miongo miwili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Je ni mkakati gani huo tegea sikio mahojiano haya kati ya mkuu wa Idhaa ya redio ya Umoja wa Mataifa Flora Nducha na Balozi Mahiga anayeanza kwa kufafania kwa nini kaenda Somalia ghafla.