Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Alihesabiwa siku za kuishi lakini akaishi zaidi

Umoja wa Mataifa unaendelea kupigia chepuo usambazaji wa huduma za kujikinga na virusi vya ukimwi, VVU ikiwa ni moja ya utekelezaji wa lengo namba 3 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Lengo hilo la ustawi wa afya kwa wote linaangazia siyo tu Malaria na Kifua Kikuu bali pia Ukimwi ambao unaendelea kuwa tishio, licha ya kwamba tayari kuna kinga. Huko nchini Kenya, mwanamke mmoja ambaye baada ya kukatiwa tiketi ya kifo, alikata tamaa akaona dunia imemgeuka. Lakini baada ya kuamua kuchukua hatua, nuru ikaingia na hata akaweza kuongeza familia yake. Je alifanya nini ?

UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Kina mama wajasiriamali waneemeka na mafuta Uganda

Upatikanaji wa bidhaa ya mafuta nchini Uganda umeleta faraja kwa mamilioni ya wananchi ambao sasa wanaona nuru ya kupungua kwa bei ya bidhaa hiyo katika siku za usoni. Na neema hiyo sio kwa waendesha magari tu bali pia kwa wafanya biashara ndogondogo au wajasiriamali wakiwemo wanawake. Mwandishi wetu wa Uganda John Kibego amewatembelea baadhi ya wanawake walioanza kunufaika na uwepo wa shughuli za uchimbaji mafuta katika eneo la ziwa Albert nchini humo ili  kupata ufafanuzi zaidi unagana naye

Picha: UNPA

Wasichana Sierra Leone wapingana na wazazi kulinda haki zao

Hebu fikiria mtoto wa kike punde tu baada ya kuzaliwa anafungwa kamba mkononi, ya kwamba ni kishika uchumba kwa kuwa tayari amepata mume. Hiyo inaweza isikuingie akilini iwapo u mkazi wa nchia ambako haki za mtoto zinazingatiwa, hata hivyo nchini Sierra Leone, hilo ni jambo la kawaida na linapatiwa msisitizo kutokana na ukatili wa kijinsia na mila na desturi potofu. Hata hivyo hivi sasa nchini humo wapo watoto wa kike na wasichana ambao wamefunguka macho na wanapingana na hata wazazi wao. Je wanafanya nini?

Sauti
4'12"

Choo chako ni salama?

Utafiti umebaini kwamba ukosefu wa vyoo safi  na salama ni hatarishi kwa afya ya binadamu. Takwimu za mashirika ya ufya ulimwenguni kama WHO na wengine zinaonyesha kuwa jamii zinazoishi katika mazingira yasiyo na vyoo salama zipo katika athari za kupatwa na milipuko ya magonjwa yatokanayo ya ukosefu wa matumizi salama ya vyoo kama kipindupindu na magonjwa mengine.

Dansi ya kitamaduni yaenziwa Uganda

Wakati shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO), linapigia chepuo utunzaji na ukuzaji wa utamaduni,  mjini Hoima nchini Uganda, waimbaji wa kitamaduni waliandaa tamasha la muziki kandoni mwa tamasha za muziki wa kisasa.

Je, lilishindana? Basi ungana na John Kibego katika makala ifuatayo...

Mpatanishi anapofungasha virago ni mashaka- Dkt. Salim

Hatma ya amani Mashariki ya Kati hususan kati ya wapalestina na waisraeli imeingia dosari baada ya Marekani kutangaza kutambua Yerusalem kama mji mkuu wa Israel. Marekani ikichukua msimamo huo nchi 128 wanachama wa  wa Umoja wa Mataifa wamepitisha azimio la kuitaka nchi hiyo ibadili uamuzi huo, uamuzi ambao unaenda mbali zaidi na kuhamisha ubalozi wa Marekani kutoka mji mkuu wa sasa wa Israel, Tel Aviv kwenda Jerusalem. Lakini nini maana ya hatua hizi? Flora Nducha amezungumza na Dkt.

Ufugaji nyuki sasa ni mtaji dhidi ya umaskini huko Kyela, Tanzania

Kupitia lengo namba moja la kutokomeza umasikini lililomo kwenye ajenda ya  maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa  ya mwaka 2030, serikali zinahimizwa kutafuta mbinu mbadala kuwawezesha wananchi kupitia miradi mbalimbali ili kujikwamua na umasikini ifikikapo mwaka 2030.

Tanzania ni nchini mojawapo ambako serikali imechukua jukumu la kutoa elimu ya SDGs kwa kutafsiri malengo yao endelevu kwa lugha ya kiswahili ili kutoa mwongozo kwa wananchi na pili kuwapatia fursa za ujasiriamali kupitia miradi  mbalimbali kama  ufugaji, uvuvi, kilimo na kadhalika.

Vijana Somalia badilisheni simulizi potofu kuhusu vijana

Nchini Somalia wiki hii wamezindua sera ya taifa ya vijana ambayo kwayo inazungumzia hatua za kukwamua vijana kuelekea utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Uzinduzi huo umefanyika wakati wa mkutano wa taifa wa vijana kwenye mji mkuu Mogadishu ukihudhuria na viongozi wa kitaifa na kimataifa. Miongoni mwao ni mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu vijana Bi. Jayathma Wickramanayake  ambaye amewasihi vijana sasa kushika usukani ili kubadili simulizi potofu ya kwamba kijana ni lazima atatumbukia kwenye misimamo mikali na kuleta ghasia.

(Picha:UN/Aliza Eliazarov)

Tumesikitishwa na kushtushwa na shambulio dhidhi ya walinda amani wetu:Mahiga

Tumeshtushwa sana na kusikitishwa na shambulio la jana dhidi ya walinda amani wetu. Amesema hayo waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika ya Mashariki wa Tanzania Balozi Augustine Mahiga alipozungumza leo na Flora Nducha wa idhaa hii kufuatia kuuawa kwa walinda amani wa Tanzania 14, wengine 38 kujeruhiwa wakiwemo walio hali mahtuti na wanne kutojulikana walipo huko Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC, baada ya kundi la waasi wa ADF kuzamia kituo cha walinda amani hao.

(MAHOJIANO KATI YA FLORA NDUCHA NA BALOZI AUGUSTINE MAHIGA)