Dkt Salim azungumzia uongozi Afrika na mustakhbali wa Sudan Kusini
Mwaka 2013 umefikia ukomo. Barani Afrika, mengi yametokea na mengine yanaendelea kutokea. Mathalani kifo cha Mzee Madiba na mzozo unaoendelea Sudan Kusini na kufanya wanadiplomasia kuendelea kukuna vichwa vyao kila uchao kupata suluhu ya kudumu za mzozo huo ndani ya taifa hilo changa lililopaswa kuwa mfano. Je nini mustakhbali wa Afrika baada ya Mandela? Na vipi Sudan Kusini?.