Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tukihifadhi mazingira leo tunaepuka gharama kubwa Kesho

Tukihifadhi mazingira leo tunaepuka gharama kubwa Kesho

Pakua

Wana mradi wa kuruwitu kutoka Kilifi Mombasa nchini Kenya, wametoa wito wa kuhifadhi mazingira leo ili kuepuka athari zake katika kizazi kijacho. Shida Magunda na Katana Ngala Hinzano wako katika mradi wa kuhifadhi mazingira ya bahari Mombasa kwa kutumia uzalishaji wa samaki. Mradi wao ambao ni wa kwanza nchini Kenya pi umetunukiwa tuzo ya mazingira ya Equator inayotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP na Equator initiative. Wamezungumza na Flora Nducha na Katana Ngala anaanza kueleza historia ya mradi

Photo Credit
Shida Magunda na Katana Ngala Hinzano katika mahojiano na Flora Nducha wa Idhaa ya Kiswahili. Picha: UM/Idhaa ya Kiswahili