Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

UN News/Assumpta Massoi

Siri ya kuwa sehemu ya tuzo hii ni ushirikiano wetu - Fr. Benedict Ayodi

Hii leo kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kumefanyika hafla la kupatia tuzo washindi wa Tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, tuzo inayotolewa kwa mtu mmoja mmoja au kundi kwa kuzingatia mchango wao kwenye kusongesha haki za binadamu. Miongoni mwa washindi wa watano ni Ushirikiano wa kimataifa wa mashirika ya kijamii, watu wa asili, harakati za kijamii na jamii za mashinani. Shirika lisilo la kiserikali la kimataifa la Wafransiskani wakapuchini ni sehemu ya ushirikiano huo.

Sauti
7'46"
UN News/George Musubao

MONUSCO na ufanikishaji wa uchaguzi mkuu wa 2023 DRC

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, (MONUSCO) unashiriki katika maandalizi ya uchaguzi mkuu nchini humo unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu ambapo tayari umeshasaidia usafirishaji wa nyaraka za uchaguzi, halikadhalika mafunzo kwa polisi wa kitaifa ili uchaguzi huo uwe huru na ufanyike kwa amani.

Sauti
4'53"
UN News

Tuna imani Tanzania tutafikia lengo la huduma za afya kwa wote 2030: Waziri Ummy

Tanzania taifa lililo Afrika Mashariki limesema limejipanga vyema katika kutekeleza azimio la kuchukua hatua kuhusu huduma za afya kwa wote lililoidhinishwa kwa kauli moja mwishoni mwa juma na nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa hapa Makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani. Waziri wa afya wa Tanzania Ummy Mwalimu alikuwa miongoni mwa waliohudhuria na ameketi chini na Flora Nducha wa Idhaa hii na kumfafanulia mikakati yao ya kutekeleza azimio hilo.

Sauti
5'52"
UN News

Msukumo dhidi ya TB ufanane na ule wa COVID-19- Waziri Wafula

Mkutano wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mapambano dhidi ya Kifua Kikuu au TB ukifanyika leo hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani, Waziri wa Afya wa Kenya Susan Nakhumicha Wafula amesema kutokomeza TB ifikapo mwaka 2030 inawezekana endapo dunia itashikamana na kuweka msokumo mkubwa kwa ugonjwa huo kama ilivyofanya wakati wa mlipuko wa janga la COVID-19. Waziri Wafula alizungumza na Flora Nducha wa Idhaa  hii ya Umoja wa Mataifa.

Sauti
8'40"
UN News

Tunaelimisha wanafunzi na vijana kuhusu mabadiliko ya tabianchi - Madina Jubilate Kimaro

Wiki hii hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kumefanyika mkutano wa tathmini ya malengo ya maendeleo endelevu SDGs kuona wapi nchi wanachama, kampuni, watu binafsi wamefikia kusongesha maendeleo hayo yanayofikia ukomo mwka 2030. Vijana nao walikuwa na siku zao mbili za kuelezea wanafanya nini kule waliko na wanataka nini kifanyike kusongesha malengo hayo likiwemo namba 13 la tabianchi. Miongoni mwa vijana walioshiriki ni Madina Jubilate Kimaro, Balozi wa Mazingira wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF nchini Tanzania.

Sauti
6'24"
UN News

Mradi wa "Football for the Goals" kufanikisha malengo 17 ya maendeleo endelevu Rwanda - UN Rwanda

Umoja wa Mataifa umekuwa ukipigia chepuo mbinu mbali mbali halali za kufanikisha malengo 17 ya maendeleo endelevu, SDGs, na miongoni mwa mbinu hizo ni mpira wa miguu, soka, wengine wakisema kabumbu au kandanda! Sasa wenyewe wabobezi au manguli wa soka wameitikia wito na Umoja wa Mataifa hususan nchini Rwanda ukaitikia Naam!!! Je nini kinafanyika? Assumpta Massoi wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa ameketi na Mkuu wa Ofisi ya Mratibu Mkazi wa UN, Rwanda Josephine Marealle-Ulimwengu na anafafanua kitendawili hicho.

Sauti
6'43"
UN Photo/Eskinder Debebe

Walinda amani wanaondoka Mali lakini Umoja wa Mataifa unabakia

Baada ya kuweko nchini Mali kwa muongo mmoja, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani na kuweka utulivu nchini humo umeanza kufunga virago. Hii ni baada ya mamlaka nchini humo kutaka ujumbe huo uondoke, ombi ambalo liliridhiwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Sasa MINUSMA inatakiwa iwe imeondoka ifikapo tarehe 31 mwezi Agosti mwaka huu.

Sauti
3'40"
UN/Anold Kayanda

Wanawake wapatiwe nafasi katika sayansi na teknolojia, watasongesha agenda 2030- Mwanaisha Ulenge

Ikiwa imesalia takribani miaka 6 ushehe kufika mwaka 2030 muda ambao ulimwengu ulijiwekea lengo la kuwa umetimiza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), mapema mwaka huu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiamini wanawake wanasayansi wana uwezo wa kuchangia haraka katika maendeleo ya ulimwengu, alieleza namna kuwanyima fursa za sayansi wanawake kunarudisha maendeleo nyuma na hivyo akashauri wanawake wanasayansi wapewe nafasi kuanzia darasani, maabara na katika vyumba vya maamuzi.

Sauti
7'17"
UN News

Ujumuishwaji ni msingi mkuu katika kusongesha malengo ya maendeleo endevu - Waheshimiwa Baraza na Mugabe

Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu lijulikanalo kama HLPF linafikia tamati hii leo hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York-Marekani. Wawakilishi wa nchi na serikali, wanasayansi, wanazuoni, mashirika ya umoja wa Mataifa, asasi mbalimbali na vijana wamekutana kuanzia tarehe 10 Julai kujadili hatua za kuchukua ili  kuhakikisha malengo hayo muhimu ya maendeleo yanatimizwa ifikapo mwaka 2030.

Sauti
8'15"