05 OKTOBA 2022
Hii leo kwenye Habari za UN tunamulika masuala ya amani na usalama, hali ngumu ya uchumi Tunisia yasababisha wananchi kutojua la kufanya, siku ya walimu duniani na uboreshaji wa madarasa huko Malawi.
1. Idadi kubwa ya matukio ya utesaji katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) vinatokea katika maeneo yaliyoathiriwa na mizozo ambako hali ya kutoadhibiwa kwa wahalifu imeenea.