Jarida 31 Januari 2022
Miongoni mwa tuliyonayo kutoka Umoja wa Mataifa
Wakimbizi wa Burundi walioishi kwa vipindi tofauti na hata miongo kadhaa ukimbizi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kwa msaada wa shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR wameanza kurejea nyumbani Burundi. Kundi la kwanza katika mwaka huu wa 2022 waeleza furaha yao kurejea nchini mwao.