29 JULAI 2022
Hii leo jaridani tunamulika pengo la huduma za ulinzi kwa wakimbizi na wasaka hifadhi wanapokuwa kwenye safari za kusaka maisha bora. Ni ripoti ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi duniani, UNHCR. Kisha tunabisha hodi Tanzania hususan mkoani Kigoma ambako shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO, limezindua Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi TAWFA kupitia mradi wake wa kukuza mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi katika ziwa Tanganyika.