23 SEPTEMBA 2022
Pakua
Hii leo kwenye Habari za UN, Flora Nducha anaanza na taarifa kutoka ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambako Rais wa mpito nchini Burkina Faso Paul Damiba anaelezea hatua walizochukua kurejesha utulivu nchini mwao.
Kisha anakwenda Turkana nchini Kenya ambako mtoto Carol mwenye umri wa miaka 11 alinajisiwa na mzee ambaye alikuwa amuoe kwa lazima lakini tukio hilo lilisambaratishwa na wapasha habari, sasa anaelekea kutimiza ndoto yake ya shule.
Makala ni kutoka jukwaa jipya la wanawake viongozi duniani likimulika changamoto za wanawake viongozi ikielezwa kuwa muda wa mabadiliko ni sasa.
Mashinani ni kauli ya Katibu Mkuu wa UN kuhusu ukanda wa Sahel. Karibu!
Audio Credit
FLORA NDUCHA
Audio Duration
11'38"