30 SEPTEMBA 2022
Hii leo katika Habari za UN Flora Nducha anamulika:
Taarifa ya kwamba hatua za kutokomeza ubaguzi dhidi ya watu wenye asili ya Afrika zinatekelezwa vipande vipande licha ya harakati zinazoendelea za kuondokana na ubaguzi wa kimfumo.
Nchini Ureno ,shirika moja lililoanzishwa na Maria Ramires linasaidia wanawake wazee kujijengea mnepo hata wakati wa utu uzima, mathalani kujifunza kuendesha merikebu zenye matanga.