Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

28 SEPTEMBA 2022

28 SEPTEMBA 2022

Pakua

Katika Habari za UN hii leo Flora Nducha anaanza na Afya ya akili miongoni mwa wafanyakazi na changamoto zake. Taarifa hii  kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa ikiwemo lile la afya ulimwenguni, WHO na ajira ILO. Mashirika yanasema ubaguzi, ukosefu wa usawa na unyanyasaji pahala pa kazi ni tatizo. Pili anakwenda Zambia kuona jinsi vituo vya maendeleo ya awali ya mtoto, ECD vimeleta tofauti chanya katika makuzi ya watoto. Makala anabisha hodi Tanzania ambako shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO limegawa maziwa kwenye shule 4 za msingi mkoani Dodoma ikiwa ni siku ya kimataifa ya unywaji maziwa shuleni, na mashinani tunasalia hapa Umoja wa Mataifa kusikia  ujumbe kutoka kwa kijana mchechemuzi wa haki kwa jamii na elimu kwa wote.

Audio Credit
FLORA NDUCHA
Audio Duration
11'31"