Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Homa ya nguruwe wa Afrika imeripotiwa kutapakaa Urusi Kaskazini, imehadharisha FAO

Homa ya nguruwe wa Afrika imeripotiwa kutapakaa Urusi Kaskazini, imehadharisha FAO

Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limetangaza ya kuwa ule ugonjwa maututi wa nguruwe, wenye kutambulika kama homa ya nguruwe wa Afrika (ASF), mnamo tarehe 20 Oktoba umegunduliwa katika eneo la St Petresburg, liliopo kaskazini-magharibi katika Urusi, kilomita 2,000 kutoka kusini ya Urusi ambapo maradhi haya yalikutikana hapo kabla.